Friday, September 21, 2012

Tanzania Inaendelea Kufedheheka

Hapa kuna ujumbe kutoka Jumuia ya Nchi za Ulaya. Ujumbe unalalamikia mauaji ya mwanahabari Daud Mwangosi. Papo hapo, kati ya mambo mengine, ujumbe unaikumbusha serikali ya Tanzania umuhimu wa uhuru wa vyombo vya habari, uhuru ambao umeendana na uhuru wa watu kujieleza. Ujumbe unaikumbusha serikali ya Tanzania kufanya kila liwezekanalo kudumisha na kuendeleza uhuru huo.

Suali langu ni hili: Kwa nini serikali ikumbushwe umuhimu wa kulinda haki za binadamu, kama vile hili ni suala gumu sana kulielewa na kulizingatia? Na kwa nini serikali yenyewe haikutambua mara moja umuhimu huo ikawa imechukua hatua muafaka, hadi ikumbushwe na nchi za nje? Hii ni fedheha kwa nchi yetu. Hapa nimeongezea tu taarifa ya suala ambalo nililiongelea siku chache zilizopita katika ujumbe huu hapa.

Ujumbe wa  Jumuia ya Nchi za Ulaya ni huu hapa:



No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...