Saturday, April 3, 2021

Kitabu Kimetua Abuja, Nigeria

Mwezi Machi 2021 umeisha vizuri kwangu. Kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, kimetua Nigeria. Nilikuwa nimempelekea Jennifer Chinyelu Ikeaba-Obiasor, aonekanaye pichani, ambaye anaishi Abuja. Huenda hii ni nakala ya kwanza kuingia Nigeria.

Jennifer alisoma kitabu akaandika maoni kwa nyakati mbali mbali:

Ni kitabu murua chenyee upeo utakaowasidia waAfrika na waMarekani.

Uzoefu wangu unaendana na karibu kila kipengele kitabuni humu. Na kitawafungua macho watu wa tamaduni zote mbili.

Ninakipendekeza kitabu hiki kwa kila mmoja, akisome kwa sababu kitamgusa.

Jennifer nami tulikutana mtandaoni wiki chache zilizopita tukiwa wafuasi wa Toyin Umesiri, mhamasishaji maarufu wa biashara baina ya Afrika na Marekani, ambaye aliwahi kufanya mahojiano nami kuhusu kitabu changu na kuhusu athari za tamaduni katika biashara baina ya waAfrika na waMarekani. Jennifer ni mjasiriamali, mwanzishi na mkurugenzi mkuu wa Chiblenders Green. Katika juhudi za kueneza shughuli zake kimataifa, anafahamu umuhimu wa kuzielewa tamaduni za wengine. Katika muda mfupi wa kufahamiana naye, amenifundisha mengi na ninamshukuru.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...