Tuesday, April 30, 2019

Maonesho ya Vitabu Blaine, Minnesota

Aprili 26-28, nilishiriki maonesho ya vitabu yaliyoandaliwa na Bukola Oriola kusherehekea miaka kumi tangu kuchapishwa kwa kitabu chake cha kwanza, Imprisoned: The Travails of a Trafficked Victim. Kwa kuwa nimeshiriki maonesho mengi ya vitabu, naweza kusema kwamba maonesho haya aliyoandaa Bukola yalikuwa ya pekoe.

Kwa uzoefu wangu, nimeona maonesho yakidumu siku moja, lakini haya ya Bukola yalidumu situ tutu. Kwa hovyo, yalitoa fursa kwa yeyote kuhudhuria siku mojawapo, ambaye hakuweza kuhudhuria siku nyingine.

Ingawa Bukola aliandaa maonesho haya kusherehekea miaka kumiss ya kitabu shake, aliwaalika waandishi wengine kushiriki. Nami niliwasilisha  vitabu vyqngu. Hakuhitaji tuwepo muda wote wa maonesho, bali wakati maalum uliopangwa kwa mwandishi moja moja kuonekana jukwaani kwa saa moja.

Nilitumia muda mrefu kiasi kwenye maonesho, tarehe 26 na 28. Nilionana na waandishi kadhaa, wakiwemo ninaowafahamu, kama vile Rita Apaloo, mwandishi wa African Women Connect: How I started and grew a networking group of African immigrant women for friendship, business, and community.

Nilikutana na kuongea na watu wengi, nikaongea nao na kubadilishana mawazo na uzoefu. Kila maonesho ya vitabu ambayo nimehudhuria yamekuwa ya manufaa sana.  Haya maonesho ya Bukola mayo yalikuwa hovyo, na anastahili kushukuriwa kea juhudi zake za kuhamasisha usomaji na kuwawezesha waandishi.



Friday, April 26, 2019

Mhadhara Wangu Yankton, South Dakota

Tarehe 19 Aprili, nilienda Yankton, jimbo la Dakota Kusini, kufuatia mwaliko kutoka kwa Michael Schumacher, mratibu wa A.M.E. Allen Church. Alinitafuta baada ya kusoma taarifa juu ya mhadhara niliokuwa nimetoa mjini Red Wing, Minnesota, kuhusu jadi ya hadithi simulizi katika Afrika I

Katika kunitambulisha kwa watu waliohudhuria, ndugu Schumacher aliwaelezea jinsi kitabu changu cha Matengo Folktales kilivyokuwa kimetajwa katika programu ya television ya Jeopardy  Hiyo ni programu maarufu hapa Marekani.
Mhadhara wangu ulihusu chimbuko na kukua kwa utamaduni na tofauti za tamaduni. Niliongelea Afrika kama chimbuko la binadamu, lugha na masimulizi, kisha nikaelea jinsi kutawanyika kwa wanadamu sehemu mbali mbali za kulivyoleta tamaduni na lugha mbali mbali.

Niltumia kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Diiferences kuainisha uhlisia na athari za kuwepo kwa tamaduni tofauti. Katika kuelezea kuzuka na kustawi kwa matumizi mbali mbali ya masimulizi nilinukuu na kuelezea methali kadhaa na halafu nikasimulia hadithi ya "The Monster in the Rice Field" iliyomo katika kitabu changu cha Matengo Folktales.

Wahudhuriaji walichangia mifano ya tofauti za tamaduni ambazo wamewahi kukumbana nazo. Mmoja alisema kwamba ni mwalimu na kwamba ana wanafunzi anaowapeleka Tanzania hivi karibuni. Nilifurahi kusikia hivyo.

Tulipomaliza kikao, watu walinunua vitabu vyangu nilivyoleta. Huyu mwalimu niliyemtaja alisema atavitumia vitabu hivi kama mwongozo kwa wanafunzi katika safari yao. Ninafurahi kwamba vitabu vyangu sasa viko katika maktaba ya AME Allen Church. Hili ni jambo kubwa, nikizingatia historia ya jengo  hili ambalo lilijengwa mwaka 1885 na watu weusi baada ya kukombolewa utumwani.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...