Mhadhara Wangu Leo Umekuwa Mzuri
Mhadhara wangu leo katika chuo cha South Central umekwenda vizuri sana. Nilijua hali ingekuwa hivyo, kwani nilikuwa naongelea masuala ambayo nina uzoefu nayo kwa miaka mingi. Niliongea na wanafunzi wakiwa mbele yangu na wengine wakiwa mji wa Mankato ila tunaonana nao kwenye skrini ya televisheni. Walimu wao walijigawa sehemu hizo mbili. Mhadhara ulikuwa juu ya kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences , ambacho maprofesa waliwaelekeza wanafunzi wakisome kabla ya mhadhara wangu. Niliibua masuala mengi, kwa muhtasari, nikianzia na uzoefu wangu kama mshauri wa programu zinazopeleka wanafunzi na watu wengine Afrika. Nilielezea nilivyoandika kitabu hiki , na changamoto zake. Hatimaye, nilitoa nasaha kuhusu mambo ya msingi ya kukumbuka tunapokutana watu wa tamaduni mbali mbali. Kipindi cha masuali na majibu kilifana sana. Nilifurahi kuona jinsi wanafunzi na maprofesa walivyokuwa wanakinukuu kitabu, hata kunikumbusha vipengele ambavyo sikuvikumbuka. Mwishoni