Thursday, September 17, 2009

Warsha: "Utamaduni, Utandawazi na Maendeleo," (Tanga, Agosti 29)


Tarehe 29 Agosti niliendesha warsha Tanga, Tanzania, mada ikiwa ni "Utamaduni, Utandawazi na Maendeleo". Warsha hii ilifanyika katika kituo kiitwacho Meeting Point Tanga na ilidumu kuanzia saa nne asubuhi hadi saa kumi na moja jioni. Hapo juu anaonekana Mama Ruth Nesje, mkurugenzi wa kituo, akinitambulisha kwa washiriki wa warsha.

Niliamua kufanya warsha hii kutokana na uzoefu wangu wa kuelezea masuala haya ya utamaduni kwenye vyuo, taasisi, makampuni, makanisa, jumuia mbali mbali na watu binafsi huko Marekani. Warsha hii ilikuwa na mvuto mkubwa kwa washiriki na iliamuliwa kuwa zifanyike warsha hizi siku zijazo. Kitu kimoja kilicholeta msisimko na mjadala mkubwa ni makala yangu "Maendeleo ni Nini?"

Ninapangia kuandika zaidi kuhusu warsha hii, na nyingine ambayo niliendesha Dar es Salaam tarehe 5 Septemba, ila nimeona niweke hii taarifa fupi hapa, kwa sasa. Kama kianzio, nimeweka picha chache zilizopigwa siku hiyo.




(Photos by Vesla Eriksen)

Thursday, September 10, 2009

Nimeonana na Mheshimiwa Michuzi


Tarehe 4 Septemba, 2009 ilikuwa siku maalum kwangu, kwani nilipata bahati ya kuonana na gwiji wa blogu, Mheshimiwa Michuzi ofisini kwake pale Mtaa wa Samora, Dar es Salaam. Hii ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuonana na gwiji huyo.

Tuliongelea mambo mengi yahusuyo blogu na mawasiliano ya kisasa kwa ujumla. Kwa mfano, alikumbushia mkutano wa wanablogu unaopangwa kufanyika Dar es Salaam mwezi Desemba mwaka huu. Nilimwona Michuzi kuwa mtu mwenye hamu ya kuona maendeleo. Hasiti kutoa ushauri wa kuwasaidia wengine. Alisema kuwa anapitia blogu nyingi, na hapo akaniambia kuwa picha iliyopo kwenye blogu yangu si nzuri. Hapo hapo aliniambia nisimame na akanipiga picha nikaiweke kwenye blogu.

Michuzi anaheshimu taaluma yake na anapenda kuona wanablogu wanasukuma mbele gurudumu la mawasiliano hayo kwa kila mmoja kutafuta kipengele maalum na kukiendeleza, iwe ni taaluma, burudani, na kadhalika. Michuzi alisema, kwa mfano, si kila mmoja anaiweza shughuli ya mwanahabari. Tuliongelea mengi, na pia tulifanya mahojiano haya hapa.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...