Monday, October 24, 2022

Mdau Amechapisha Mapitio ya Kitabu Changu

Tarehe 21 Oktoba, 2022, katika gazeti la The Citizen, Neelam Babul alichapisha mapitio ya kitabu changu. Nimevutiwa na mrejesho wake. Msomaji yeyote anayetoa maoni yake juu ya kitabu changu, yawe maoni ya ainna yoyote, nashukuru.

Saturday, October 1, 2022

Nimekutana na Wasomaji Wangu

Leo mjini Burnsville, Minnesota, nilikutana na wasomaji wangu wawili: Sarah B. Kamsin mwenye asili ya Sudan ya Kusini na Brighid McCarthy kutoka Marekani. Sarah ndiye aliyeandaa mkutano.

Sarah na mimi tumefahamiana tangu Julai 2019, aliponikuta kwenye maonesho ya vitabu mjini Blaine, Minnesota, akaipatia kitabu cha "Africans and Americans: Embracing Cultural Differences." 

Baadaye Sarah alichapisha kitabu cha mashairi yake kiitwacho  "Vita, Babel, Cauliflower," ambacho nilikisoma nikakifurahia, na kisha nikakiandikia uhakiki. Unaweza kuona kisehemu cha uhakiki wangu kwenye tovuti ya Amazon. Sarah ana kipaji kikubwa cha utunzi wa mashairi ya kiIngereza.

Katika maongezi yetu ya leo, nimefahamu kuwa baada ya kusoma kitabu changu cha "Africans and Americans: Embracing Cultural Differences," Sarah  alianza kumwelezea rafiki yake wa miaka mingi Brighid juu yangu na kitabu hiki..

Kutokana na hayo, Brighid alifurahi sana kukutana nami leo. Alikuwa na nakala ya kitabu, kikiwa kimepigiwa mistari kwenye vifungu na sentensi nyingi, kuashiria kuwa amekuwa akisoma kwa uangalifu na tafakuri tele. Nilishangaa anavyokumbuka hata mambo madogo yaliyomo kitabuni.

Tuliongea kwa masaa matatu, na muda mwingi tuliongelea tofauti za tanmadunni nilizozielezea kitabuni. Lakini pia tuliongelea uwezekano wa kushirikiana katika utatuzi wa mahitaji mbali mbali katika jamii za Afrika Mashariki, kama vile elimu na maji. Tumefurahi kugundua kuwa wote tayari tumekuwa tukifanya hayo. Brighid, kwa mfano amekuwa akifanya shughuli hizi Arusha. Tumehamasika kufanya zaidi.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...