Monday, December 23, 2013

Nimepata Zawadi Murua ya Krismasi Leo

Wafuatiliaji wa fasihi ya ki-Ingereza wanafahamu kuwa juzuu la pili la barua za Hemingway, limechapishwa mwaka huu. Sawa na juzuu la kwanza, hili ni buku kubwa, kurasa 519.

Leo nimepokea kifurushi kutoka Amazon.com. Binti yangu Zawadi aliponiletea nilishangaa, maana sijaagiza kitabu kutoka Amazon kwa miezi kadhaa. Nilipofungua kifurushi sikuamini macho yangu. Ni juzuu hilo nililolitaja. Nimefurahi sana. Nilikuwa natamani kufanya mkakati wa kununua. Lakini Mungu mkubwa, kamwongoza huyu bwana aninunulie hiki hiki ambacho roho yangu ilikuwa inatamani.

Bwana aliyeniletea ni David Cooper, mzazi wa mwanafunzi mmojawapo wa wale waliokuja Tanzania mwezi Januari mwaka huu kwenye kozi ya Hemingway. Baba huyu ni msomaji makini wa Hemingway na waandishi wengine.

Ni huyu bwana, anayeishi Ohio, alipoambiwa na kijana wake kwamba natamani siku moja kwenda Montana kuongea na Mzee Patrick Hemingway, mtoto pekee wa Ernest Hemingway aliebaki, alisema atatusafirisha kwa ndege yake.

Siku ilipofika, yeye na rubani wake walifika Minnesota, wakatuchukua, mimi na wanafunzi wawili, akiwemo yule kijana wake.

Bwana huyu ni kama tumejenga urafiki. Namshukuru sana.
 

Wednesday, December 18, 2013

Mama Kutoka Togo Kawahi Kununua Zawadi za Krismasi

Mama mmoja kutoka Togo ambaye ni rafiki ya familia yangu, alitutembelea wiki kama tatu zilizopita. Kati ya mambo mengine, alsema anataka kununua nakala mbili za kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Alisema ni zawadi ya Krismasi kwa marafiki zake waliopo hapa hapa Marekani.

Huyu mama ni kati ya wasomaji wa mwanzo kabisa wa kitabu hiki mara kilipochapishwa, mwanzoni mwa mwaka 2005. Alikipenda sana na kuanzia pale akawa anakipigia debe kwa watu mbali mbali. Hata kuna wakati ndugu yake alikuja kutoka Togo, akamtafutia nakala, ambayo alienda nayo Togo.

Namshukuru mama huyu. Nanatafakari suala hilo. Kuna vitabu vingi sana hapa Marekani ambavyo vinafaa kama zawadi kwa ndugu na marafiki. Lakini mama huyu kachagua kitabu changu. Halafu huyu mama hana kibarua au kipato cha ajabu: anafanya kazi ya kutunza wazee hospitalini.

Lakini, mama huyu, pamoja na ugumu wa kupata hela hapa Marekani, pamoja na ugumu wa matumizi kwa ujumla, kabana hela akaamua kununua vitabu hivi. Halafu, mteja anapokurudia tena, kwa hiari yake, ni jambo la kushukuru, kwamba aliridhika au alifurahishwa na kile alichokipata mwanzo kutoka kwako. Kwa vile mama huyu ni mpiga debe wangu makini, nilimpa punguzo zuri la bei.

Nimeona tabia hii ya kununua vitabu miongoni mwa wa-Afrika wa nchi zingine, ila sio Tanzania. Kwa mtazamo wangu, hao wenzetu wanatoka nchi ambazo zimewaelimisha.

Niliwahi kuandika makala katika blogu hii kuhusu suala la kumpa mtu kitabu kama zawadi ya Krismasi au Idd El Fitr. Mawazo niliyotoa bado ninayo vile vile vile.

Tuesday, December 10, 2013

Kwa Wapumbavu wa Kigoma Wanaoleta Vurugu Kwenye Mikutano ya Dr. Slaa

Huu ni ujumbe kwenu wapumbavu wa sehemu mbalimbali za Kigoma ambao mmekuwa mkileta vurugu kwenye mikutano ya Dr. Slaa, katibu mkuu wa CHADEMA.

Ni moja ya haki za binadamu kutafuta, kupata, au kusambaza taarifa na mitazamo katika masuala mbali mbali yanayoihusu jamii. Someni tangazo la kimataifa la haki za binadamu. Taarifa hizo hupatikana kwa namna mbalimbali, kuanzia vyombo vya habari hadi mikutano.

Nimeona picha za makundi ya watu wakiwa wamekusanyika kumsikiliza Dr. Slaa. Hiyo ni haki yao, mojawapo ya haki za binadamu. Lakini nimeona pia taarifa za wapumbavu wachache, kama vile Kasulu, wakija kuvuruga au kujaribu kuvuruga mikutano hiyo. Hao ni wapumbavu. Kenge wakubwa.

CCM, chama ambacho kimeshika hatamu katika nchi hii, chenye wajibu wa kuongoza na kuelimisha jamii, kimekaa kimya. CCM naijumlisha katika kundi hili la wapumbavu. Zito Kabwe, ambaye anatajwa na hao wavurugaji kwamba wanamtambua yeye, naye hajasema kitu. Naye ni mpumbavu.

Kuna haki zingine za binadamu zinazohusika katika suala hili. Moja ni haki ya kila binadamu kukusanyika na kujumika na wengine kwa amani. Nyingine ni haki ya kila raia kwenda popote katika nchi yake. Wapumbavu wa Kigoma mjini waliomtishia Dr. Slaa asikanyage Kigoma wakapimwe akili.

Mimi sio mwanachama wa chama chochote cha siasa. Ila nakerwa na upumbavu nilioelezea.

Monday, December 9, 2013

Wajinga Hunena, CCM Ilileta Uhuru Tanganyika

Kiwango cha ujinga Tanzania kinatisha. Utawasikia wengi wakisema kuwa CCM ilileta Uhuru Tanganyika mwaka 1961. Wajinga wengine, kuanzia wanasiasa hadi watu wa mitaani, husema kuwa CCM imekuwa madarakani kwa miaka 52.

Utamsikia mwanasiasa anaiponda CCM kwa kuuliza, "Miaka yote 52 ya utawala wa CCM, wananchi mmenufaika vipi?" Na utammsikia kada wa CCM akitamba, "CCM ni chama chenye uzoefu wa miaka 52.

Hapakuwa na CCM mwaka 1961. Chama kilicholeta Uhuru Tanganyika ni TANU. Wala CCM haijawa madarakani miaka 52. Kuna mengi katika historia ya Tanganyika na Tanzania ambayo yanasahaulika au kupotoshwa kwa sababu ya uzembe wa wa-Tanzania.

Wajinga wengine wanasema kuwa leo tunasherehekea kumbukumbu ya Uhuru wa Tanzania au Tanzania Bara. Mwaka 1961 hapakuwa na nchi iliyoitwa Tanzania wala Tanzania Bara. Nchi iliyopata Uhuru mwaka ule ni Tanganyika. Inasikitisha.

Monday, December 2, 2013

Ninayo Pia Blogu ya Ki-Ingereza, Jamani

Wadau wa blogu hii ya hapakwetu, samahani kama sikuweka wazi tangu mwanzo kuwa ninayo pia blogu ya ki-Ingereza. Inaitwa "Mbele" na anwani yake ni hii: http://www.josephmbele.blogspot.com.

Niliamua kuanzisha na kuendesha blogu hii ya ki-Kiingereza ili kuchangia elimu hasa katika masuala ya fasihi ya ki-Ingereza. Mimi ni mwalimu wa somo hili mwenye uzoefu tangu miaka ya mwanzoni ya sabini na kitu. Nilifundisha katika idara ya Literature, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia mwaka 1976, nikasomea shahada ya udaktari Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, Marekani, 1980-86, na kuanzia mwaka 1991 nimekuwa nikifundisha katika idara ya ki-Ingereza ya chuo cha St. Olaf hapa Marekani.

Katika blogu hii ya "Mbele" mara kwa mara ninaongelea vitabu, hasa vitabu vya fasihi. Uchambuzi wangu vitabu hivi unasomwa duniani kote. Nimeona kuwa uchambuzi wangu wa riwaya ya The Old Man and the Medal unapitiwa kuliko andiko jingine lolote na watu kutoka duniani kota.

Nina uzoefu na ufahamu mkubwa sana katika masomo hayo, na ndio nikaona niwamegee wanajamii angalau kiasi, kwani blogu si mahala pa kuandika makala ndefu, wala kitabu. Nilivyoanzisha blogu hii ya ki-Ingereza niliwawazia kwa namna ya pekee vijana wa Tanzania.

Nikiongea kwa ujumla kuhusu wa-Tanzania, ni kwamba wale wanaodhani wanajua ki-Ingereza, bado wana safari ndefu. Mimi mwenyewe naendelea kujifunza undani wa ki-Ingereza, ingawa waandishi maarufu hapa Marekani kama vile Mzee Patrick Hemingway na Jim Heynen wanapenda ninavyoandika. Ni jambo baya sana kuridhika na kile unachodhani unajua, na ndio maana nafanya juhudi.

Ninaandika ki-Ingereza sahihi, ipasavyo, na nilitegemea kuwa yoyote anayeisoma blogu ya Mbele kwa makini ataona mfano wa uandishi bora wa ki-Ingereza. Ninafahamu ninachosema, kwani kama nilivyotamka, mimi nafundisha ki-Ingereza katika chuo hapa Marekani. Lakini bado nahangaika kuboresha ujuzi wangu kwa kusoma sana na kuandika sana.

Nimeandika ujumbe huu kwa sababu mbili zinazohusiana. Hutokea mara moja moja mdau akaniuliza blogu yangu nyingine anwani yake ni ipi. Pili, nimegundua kuwa kuitaja tu katika orodha ya blogu niliyoweka hapa kulia, haitoshi. Soma pia makala hii hapa.

Wednesday, November 13, 2013

Kitabu Kinapendwa

Tangu nichapishe vitabu vyangu mtandaoni, ninaweza kufuatilia mauzo kila siku. Nimefungua duka mtandaoni, na nimetoa ushauri kwa waandishi wengine, hasa wa-Tanzania, kuhusu uzuri na ubora wa tekinolojia hii.

Ushauri wangu nimeutoa katika kitabu kiitwacho CHANGAMOTO: Insha za Jamii. Lakini inaeleweka kuwa ukiwa na wazo ukaliweka kitabuni, usitegemee kama wa-Tanzania wataliona. Huu ni ukweli ambao umesemwa tena na tena. Nami sidhani kama nina la kuongeza. Papo hapo, falsafa yangu ni kuwa ukiwa na jambo la manufaa, waeleze wengine.

Kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences ndicho chenye mauzo kuliko vingine vyote. Kila ninapoona kimenunuliwa, najiuliza ni nani huyu aliyenunua. Pengine inakuwa ni nakala moja, lakini pengine ni nakala za kutosheleza darasa. Nami sijui ni nani kaagiza. Hiki kitendawili kinanifanya niwe na dukuduku, na nafahamu kuwa sitapata jawabu.

Kuna wakati zinapita siku nyingi kidogo bila mtu kukinunua, lakini wakati mwingine hali hubadilika ghafla. Kwa mfano, Oktoba 31, niliona mtu kanunua nakala 51. Laiti ningemfahamu. Ningempelekea barua ya shukrani na pia nakala ya bure kama kifuta jasho. Lakini simjui. Ni kitendawili.

Namshukuru Mungu kwa jinsi alivyoniwezesha kuandika na kuwagusa walimwengu kiasi hicho. Yote ni uwezo wake.


Saturday, November 9, 2013

Nimenunua "Nomad," Kitabu cha Ayaan Hirsi Ali

Miaka kadhaa iliyopita, nilianza kusikia jina la Ayaan Hirsi Ali, mwandishi kutoka Somalia, ambaye alikuwa ameikimbia nchi yake na alikuwa anaishi Uholandi, ambako alifanikiwa hata kuwa mbunge. Ilionekana ni mwandishi mkorofi, kwa maana ya kwamba wengi walikerwa na kukasirishwa alivyokuwa anahoji utamaduni wa wa-Somali na u-Islam, hasa kuhusu masuala ya haki za wanawake.

Nilisoma kuhusu kitabu chake Infidel, ambacho kilisemekana kiliwakasirisha wa-Islam wengi. Nilikuwa na dukuduku ya kusoma maandishi yake, lakini, kutokana na majukumu mengi, sikufuatilia.

Hata hivi, nimezingatia ukweli kuwa, kuliko kutegemea ya kuambiwa, muhimu mtu kujisomea mwenyewe. Leo nimenunua kitabu cha Ayaan Hirsi Ali kiitwacho Nomad. Ingawa ninasoma vitu vingi kila siku, nitakipa kitabu hiki kipaumbele. Wakati huo huo, nitanunua vitabu vyake vingine. Insh'Allah, nitapata wasaa wa kuelezea nawazo yake.

Tuesday, October 29, 2013

Nimepata Wageni Leo

Leo nimepata bahati ya kutembelewa na wageni wawili. Mmoja ni Mchungaji John Mhekwa kutoka Tungamalenga, Iringa. Mwingine ni Profesa Paula Swiggum wa chuo cha Gustavus Adolphus, St. Peter, Minnesota.

Mchungaji Mhekwa hatukuwa tunafahamiana, lakini Profesa Swiggum tumefahamiana kwa miaka kadhaa, kwani katika programu yake ya kupeleka wanafunzi Tanzania, alinialika kuongea nao kuhusu masuala ya tofauti za tamaduni, kama maandalizi ya safari.

Wanafunzi walikuwa wanasoma kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Huo ulikuwa ni uamuzi wake. Mazungumzo yangu na hao wanafunzi yalihusu mambo niliyoandika katika kitabu hiki. Baada ya Profesa Swiggum kustaafu, profesa aliyemrithi, katika kuendesha programu hiyo, Barbara Zust, aliendelea na utaratibu huo.

Kifupi ni kwamba Profesa Swiggum tumeanza zamani kiasi kushirikiana katika nyanja hizo. Leo ilikuwa fursa ya pekee ya kufahamiana na huyu mgeni mwingine, Mchungaji Mhekwa. Nimemwambia kuwa Tungamalenga nilipita, mwezi Agosti mwaka 2011, nikiwa na wanafunzi tukiwa tunaelekea hifadhi ya Ruaha.

Sunday, October 13, 2013

Tamasha la Vitabu Twin Cities, Oktoba 12, Lilifana

Tamasha la vitabu, Twin Cities Book Festival, lililofanyika mjini St. Paul, Minnesota, jana, tarehe 12, lilienda vizuri. Niliondoka mapema asubuhi, yapata saa mbili, nikafika kwenye maaonesho saa tatu. Sikuwa nimechelewa, kwani wakati naandaa vitabu vyangu kwenye meza yangu, wengine nao walikuwa wakiandaaa, ingawa wengi walishapanga vitabu vyangu siku iliyotangulia
Meza niliyopata, baada ya kulipia dola 80, ilikuwa namba 12. Nilikuwa nimejisajili kwa jina la Africonexion, ambayo kampuni yangu ndogo inayohusika na uchapishaji na uuzaji wa vitabu vyangu, na pia kuratibu mihadhara yangu ya kuchangia maelewano baina ya watu wa tamaduni mbali mbali. Tangu nilipoisajili kampuni hii, shughuli zake zimekuwa zikifanyika zaidi hapa Marekani, lakini hatimaye, hasa nitakaporejea Tanzania baada ya kustaafu hapa Marekani, nataka kuijenga kampuni hii Tanzania, Africa Mashariki, na sehemu zingine.







 




Kama kawaida, watu walianza kuingia ukumbini tangu milango ilipofunguliwa. Ukiwaangalia wanavyojishughulisha kuangalia vitabu kwenye meza mbali mbali, unaona kabisa kuwa hao ni watu wanaothamini elimu. Kwa vigezo vyangu, hao ni watu walioelimika.











Inavutia kuona jinsi watu wanavyoacha shughuli zao nyingine ili kuja kwenye tamasha la vitabu. Ingekuwa ni Tanzania, watu hawangehudhuria. Hilo nimeshuhudia tena na tena, na nami, na wengine wengi, tumeandika sana kuhusu suala hilo. Kadiri miaka inavyopita, Tanzania inazidi kuwa taifa la wajinga. Hakuna sababu ya kubembelezana; ukweli lazima usemwe.









Ushahidi wa kuelimika ni kuwa na kiu isiyoisha ya kujifunza mambo. Ni dukuduku ya kutaka kujua, ambayo kwa ki-Ingereza huitwa "intellectual curiosity." Mtu asiye na "intellectual curiosity" hajaelimika, kwa sababu kuridhika na kile ambacho unadhani unajua, ambacho kwa kweli ni kidogo, ni ujinga. Ni wajibu wangu kama mwalimu kupambana na tabia za aina hiyo, bila kumwonea aibu mtu yeyote.








Kama kawaida, ushiriki wangu katika tamasha la Twin Cities Book Festival ulikuwa na mafanikio mazuri. Nilionana na kuzungumza na watu wengi waliofika kwenye meza yangu. Niliuza vitabu kadhaa. Niliitangaza kampuni ya Africonexion kwa kuwagawia watu chapisho la ukurasa moja ambalo linaelezea shughuli zake, na pia niliwapa kadi ya biashara ya Africonexion.

Binti yangu Zawadi alifika baadaye kunisaidia kwenye meza yangu, nami nikapata fursa ya kutembelea meza za wachapishaji na waandishi wengine. Nilielimika sana kwa kuongea na watu mbali mbali, kujionea shughuli za uchapishaji na maelfu ya vitabu vilivyokuwepo kwenye maonesho. Nilipata fursa ya kuwaelimisha wengine, kama mwalimu, mwandishi na mshauri katika masuala ya tofauti za tamaduni na athari zake.

Tuesday, October 8, 2013

Vijana Washikwa Mtwara Wakiwa Katika Mafunzo ya Al Shabaab na Al Qaida

1 
Stori ambayo ilishika namba 1 kwenye habari 10 za AMPLIFAYA ya Clouds FM October 7 2013 ni hii ya Polisi Mtwara kukamata vijana 11 ambao walikua wakifanya mazoezi ya kijeshi waliyokua wakijifunza kutoka kwenye cd za magaidi zilizokua na mafunzo kutoka kwa makundi ya Al Shabaab na Al Qaeda.
Taarifa zaidi unaweza kuzisoma hapo chini kwenye hiyo taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi.
2 3

4 5 6


CHANZO: dj sek

0 comments:


Post a Comment

Tamasha Kubwa la Vitabu, Twin Cities, Oktoba 12

Lile tamasha maarufu kabisa la vitabu ambalo limefanyika mjini Minneapolis kwa miaka mingi, mara moja kwa mwaka, limekaribia kabisa. Kuanzia mwaka jana, tamasha limehamia mjii St. Paul, kwenye viwanja vya State Fairgrounds.

Hakuna tamasha kubwa zaidi ya hili katika eneo hili la Minnesota na majimbo ya jirani. Wanahudhuria watu yapata 7,000, wapenzi wa vitabu. Wanakuwepo waandishi, wachapishaji, wahariri, wachora picha za vitabuni, wahakiki, wauzaji wa vitabu na majarida. Wanahudhuria wazee, watu wazima, vijana, na watoto.

Nimeshiriki tamasha hili kwa miaka mingi, kama mwandishi wa vitabu na mwelimishaji katika chuo kikuu na jamii. Kila mara nimepata fursa ya kuongea na wasomaji wa maandishi yangu na watu ambao sijawahi kuwafahamu kabla. Wanakuja na maoni, taarifa, na uzoefu mbali mbali. Tunabadilishana mawazo. Inakuwa ni kama shule muhimu sana. Tamasha linapoisha, jioni, najiona nimeelimika sana.

Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuandika vitabu na maandishi mengine. Namshukuru kwa namna ya pekee kwa kuniwezesha kuandika kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, ambacho najua kimesomwa na bado kinasomwa na maelfu ya watu hapa Marekani, ambao huguswa na mawazo na ushauri niliotoa katika kitabu hiki.

Kwenye kila tamasha, ambamo kunakuweko vitabu maelfu kwa maelfu, unawajibika kushangaa wadau wanafikiaje uamuzi wa kununua kitabu fulani au vitabu fulani. Nina bahati kuwa kitabu changu, ingawa kimekuwepo sokoni kwa miaka mingi kiasi, hakijachujuka bali kinawavutia wateja. Ninachoweza kusema ni kimoja, kwamba yote ni mipango ya Mungu.

Baadhi ya watu ninaokutana nao ni waandishi chipukizi. Huniulizia namna ya kuchapisha kitabu. Nami huwahamasisha kufuatilia hali ya uchapishaji wa leo, unaotumia tekinolojia tofauti na zile tulizozizoea. Kwa taarifa, na kwa manufaa ya watu wanaoongea ki-Swahili, nimetoa maelezo na uzoefu wangu kuhusu uchapishaji huo na mikakati mingine inayohusika, katika kitabu changu cha CHANGAMOTO: Insha za Jamii.

Nimeshajiandaa vizuri kwa tamasha la tarehe 12. Nakala za vitabu vyangu ninazo, pamoja na matangazo na machapisho mengine. Nangojea kwa hamu kukutana na kuongea na watu wengi. Kwa namna ya pekee, nangojea kuongea na watoto. Insh'Allah, nitaandika ripoti ya tamasha, kama ilivyo jadi yangu. Kwenye tamasha hili, nimejisajili kwa jina la kampuni yangu ndogo iitwayo Africonexion: Cultural Consultants, ambayo nimekuwa nikijitahidi kuitambulisha Tanzania. Unaweza kuona jina hilo katika orodha ya wauza vitabu, ambayo hi hii hapa.

Thursday, September 12, 2013

Wa-Tanzania Tusiwachokoze Wanya-Rwanda

WaTanzania tunapaswa kuwa waangalifu sana tunapoongea na Wanya-Rwanda au tunapowaongelea. Hao ni watu ambao wamepitia majanga ambayo waTanzania hatuwezi hata kufikiria.

Wengi wao wameshuhudia ndugu, jamaa, marafiki wakiuawa kikatili. Wengi wameshuhudia familia yao yote ikichinjwa kwa mapanga. Wengi waliachwa wakiwa wakiwa tangu utotoni. Majanga yaliyowapata, sisi waTanzania hatujawahi kushuhudia katika maisha yetu, na hata tukijaribu kufikiria, tutakuwa tunaelea hewani tu. Undani wake na ukweli wake hatutaweza kuuelewa.

Wa-Tanzania tunashangaa kwa nini wanya-Rwanda wamepandisha jazba sana kutokana na ushauri wa Rais Kikwete kwamba wafanye mazungumzo na wapinzani wao walioko Kongo. Hatuelewi kwa nini ushauri uliotolewa kwa nia njema, kwa vigezo vyetu, umewatibua kiasi hicho. Wa-Tanzania wengi wameamua wanya-Rwanda wamevuka mpaka katika msimamo wao.

Ninaamini wa-Tanzania tunakosea katika kudhani hivyo. Angalia Israel. Mauaji ya kimbari yaliyowapata wa-Yahudi miaka ya elfu moja mia tisa arobaini na kitu hawajasahau hata chembe. Na mtu asithubutu kuwagusa kwa hilo; atatonosha vidonda na kuamsha jazba kali kuliko maelezo.

Hapa Marekani, kwa mfano, kila mtu, kila kiongozi wa serikali, anaogopa kulipuuzia au kulifanyia mzaha tukio la mauaji yale ya kimbari. Hakuna anayethubutu kuwashauri wa-Yahudi wafanye mazungumzo na yeyote ambaye ni mhusika au mtetezi wa mauaji yale. Hakuna mtu anayeweza kushinda urais hapa Marekani kama hathibitishi wazi wazi kuwa atasimama sambamba na Israel kama rafiki.

Wa-Yahudi waliunda kitengo cha utafiti cha Simon Wiesenthal, ambacho kazi yake kubwa ni kuwasaka na kuwanasa wote waliohusika na mauaji yale. Kitengo hiki kimefanya kazi sana na kinaogopwa kwa umakini wake katika kuwasaka na kuwanasa watuhumiwa popote duniani. Hisia za wa-Yahudi kuhusu mauaji ya kimbari yaliyowapata, ni kama vile yalitokea mwaka uliopita.

Ingawa wanya-Rwanda hawajaunda kituo kama hiki cha Simon Wiesenthal, sina shaka kwamba hisia zao ni sawa na zile za wa-Yahudi. Ni kitulizo cha aina fulani kwamba mahakama ya kimataifa ya mauaji ya kimbari imesaidia na inaendelea kusaidia kufanikisha jukumu la kuwasaka na kuwafikisha mahakamani wahusika au watuhumiwa wa mauaji ya kimbari.

Nimeona nitumie mfano huu wa wa-Yahudi, ili kufafanua ushauri wangu kwamba wa-Tanzania tuwe waangalifu sana tunapoongea na wanya-Rwanda.  Kitu tunachokiona sisi ni kidogo, kwao ni janga la kutisha kuzidi jinamizi lolote. Tahadhari hii inapaswa izingatiwe hasa na vyombo vyetu vya habari.

Wednesday, August 28, 2013

Zawadi Baada ya Mhadhara Finland

Bado nina mengi ya kusema kuhusu safari  yangu ya wiki iliyopita nchini Finland, kwenye mkutano. Nina kumbukumbu nyingi, na kama nilivyowahi kusema zamani, blogu yangu ni mahali ninapojiwekea mambo yangu binafsi.

Kama nilivyotamka, nilialikwa kutoa mhadhara maalum, ambao hapa Marekani huitwa "keynote address." Mada yangu ilikuwa "The Epic as a Discourse on National Identity."

Baada ya kutoa mhadhara, mtoa mhadhara alikuwa anakabidhiwa ua. Ua hilo ni shukrani ya waandaaji wa mkutano.










Hapa kushoto anaonekana Profesa Pekka Hakamies, mwenyekiti wa kamati ya maandilizi, ambaye aliniletea mwaliko.

Tulioalikwa kutoa hiyo mihadhara maalum tulikuwa watano, kila mtu akatoa mhadhara wake kwa wakati tofauti. Mhadhara wa aina hiyo hutolewa mbele ya washiriki wote wa mkutano, na unategemewa kuweka msingi au changamoto za kujadiliwa na washiriki katika vikao mbali mbali ambamo mada mbali mbali hutolewa.

Katika kuhudhuria hivyo vikao vya baadaye, nilifurahi kuwasikia washiriki mara kadhaa wakinukuu yale niliyoyosema. Katika taaluma, haya ni mafanikio. Wazo hili linaweza kuwa gumu kwa wa-Tanzania wengi kulielewa, kwani wanadhani mafanikio ni pesa. Kama huna pesa, wa-Tanzania hao wanakushangaa ukiwaambia umefanikiwa.
 
Jambo linalofurahisha pia ni kuwa unapokuwa umealikwa kama nilivyoalikwa, halafu ukachangia mkutano kwa ufanisi, unakuwa umewahakikishia waandaaji kuwa hawakukosea kukualika, na unakuwa umewaridhisha washiriki kwa kuwapa mawazo na fikra mpya.

Ni fursa pia ya kukitangaza chuo chako. Nilipokuwa mwajiriwa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kuanzia mwaka 1976 hadi 1990, shughuli zangu hizi zilikuwa zinakitangaza chuo kile. Lakini kuanzia mwaka 1991, nilivyoondoka kabisa kutokana na mizengwe ya pale, nimeridhika kabisa kuwa mwajiriwa wa Chuo cha St. Olaf na kukitangaza.

Tofauti na fikra au hisia za wa-Tanzania wengi, sijabadili uraia, na sitabadili, wala sijawahi hata kuwazia kwa namna yoyote kuchukua uraia wa Marekani. Badala yake, nimejitafutia njia kadhaa muhimu za kuitumikia nchi yangu kwa kutumia fursa za hapa ughaibuni.

Sunday, August 25, 2013

Ziara Yangu Finland Imefanikiwa Sana

Tarehe 19 hadi 24 nilikuwa kwenye Chuo Kikuu cha Turku, Finland, kwenye mkutano wa kitaaluma. Nilialikwa nikatoe mmoja ya mihadhara maalum, "keynote address." Mhadhara wangu ulikuwa "The Epic as a Discourse on National Identity." Utafiti, ufundishaji na uandishi wangu kuanzia kwenye mwaka 1977 umekuwa zaidi kuhusu masimulizi kama yale ya Iliad, Odyssey, Dede Korkut, Sundiata, Liongo Fumo, Kilenzi, Beowulf, Gassire, Ibonia, na Kalevala. Anayeonekana pichani kulia, ni Profesa Pekka Hakamies, mwenyekiti wa jopo la maandalizi, aliyenialika. Washiriki walikuja kutoka pande mbali mbali za dunia.






Hapa kushoto niko mbele ya kanisa moja, mjini Turku. Sikupata muda wa kuingia ndani, bali nilikuwa napita hapo nje kila nikiwa njiani baina ya hoteli nilyofikia na sehemu ya mkutano, mwendo wa dakika kama 15 kwa mguu.
















Jioni ya tarehe 23 nilialikwa Helsinki, kwa chakula cha jioni. Hapo nilikutana na wa-Tanzania kadhaa waliokuja kujumuika nami. Ukarimu wao sitausahau.












Friday, August 16, 2013

Nangojea Kukaguliwa "Eapoti"

Wadau, wiki ijayo ninasafiri kwenda Finland, kwenye mkutano, nikitokea uwanja wa ndege wa Minneapolis. Sasa kuna haka kasuala ka waBongo kukaguliwa sana kwenye hivyo viwanja vya ndege. Nasubiri zamu yangu.

Hii mijitu iliyotufikisha hapa imetuhujumu sana waBongo. Nasikia mingine ni mijitu mikubwa serikalini, na mingine eti ni mifanyabiashara. Biashara gani hii kama si uroho wa fisi, ujambazi, na uuaji?

Hii mijitu imechangia kuathirika kwa afya na maisha ya wengi nchini, na kinachoudhi ni kuwa inaachwa iendelee kutanua na kufanya hujuma hizo. Haya ni baadhi ya matunda ya kuwa na CCM madarakani. Nchi hii iko mikononi mwa CCM. Nawapongeza wana-CCM na vikofia vyao, na magwanda yao ya kijani, kwa kutufikisha hapa tulipo.

Miaka yote iliyopita, nilikuwa najivunia kuwa m-Tanzania, kutokana na kazi kubwa aliyofanya Mwalimu Nyerere. Ilikuwa ni heshima kuwaambia watu popote duniani kuwa mimi ni m-Tanzania. Miaka hii ya leo najisikia aibu kuwa m-Tanzania.

Sunday, August 11, 2013

Afrifest 2013 Ilifana Minnesota

Jana, mjini Brooklyn Park hapa Minnesota, yalifanyika maonesho ya Afrifest. Afrifest ni tamasha linalofanyika mara moja kwa mwaka, likiwajumuisha watu wenye Asili ya Afrika na wengine wowote wale, kwa lengo la kufahamiana, kujielimisha, na kujipatia burdani mbali mbali. Watu wa kila aina walishiriki, wazee, vijana, na watoto.

Hapa kushoto tunawaona watoto wakiwa na mpiga ngoma maarufu hapa Minnesota. Aliwaonyesha namna ya kupiga ngoma, na pia aliwaelezea maana na matumizi ya ngoma katika tamaduni za Afrika.










Watu walikuwa wameambiwa kuwa tamasha lilipangiwa kuanza saa sita mchana. Kuanzia hapo watu walikuwa wanafika, kwa wakati wao.

























Vijana kutoka benki ya Wells Fargo walifanya kazi nzuri ya kujitolea, kuwahudumia waliohudhuria. Walikuwa wamevalia tisheti nyekundu.













Hapa ni banda ambapo watu walikuwa wanajipatia chakule. Wahusika wanajua sana kuandaa vyakula, kama vile wali na kuku.











Siku nzima, kulikuwa na muziki kutoka sehemu mbali mbali za Afrika. Vibao vya akina Diamond na Mr. Nice kutoka Tanzania vilisikika.














Hapa naonekana kwenye meza yangu nikiwa na vitabu vyangu. Nimekaa na mdau wangu wa siku nyingi, Ndugu Nyangweso.

Mimi kama mwalimu, mchango wangu mkubwa katika siku ya Afrifest ni kuelimisha umma kuhusu historia na masuala mbali mbali ya watu wenye asili ya Afrika, kuanzia chimbuko la binadamu Afrika, hadi himaya mbali mbali zilizojitokeza Afrika, biashara ya utumwa ndani na nje ya Afrika, ukoloni, harakati za uhuru, changamoto za leo na fursa za siku za usoni.




Yapata saa 10 na nusu alasiri, kama taarifa zilivyokuwa zimeelezea, Mheshimiwa Al Franken, seneta kutoka Minnesota, alijitokeza kwenye tamasha. Kulitokea msisimko mkubwa, kwani kila mtu alitaka kumsalimia na kuongea naye. Picha nyingi zilipigwa, ambazo ni kumbukumbu nzuri.

Friday, August 9, 2013

Afrifest 2013, Minnesota

Kesho, Agosti 10, ndio ile siku ya tamasha la Afrifest hapa Minnesota. Ni tamasha linalofanyika mara moja kwa mwaka, kwa lengo la kuwakutanisha watu wenye asili ya Afrika na wengine pia. Afrifest ni fursa ya kufahamiana, kuelimishana, na kuburudika na maonesho mbali mbali ya michezo na tamaduni.

Kwa taarifa zaidi kuhusu tamasha la kesho, angalia tangazo nililobandika hapa. Pia soma nilivyoandika katika blogu yangu ya ki-Ingereza.

Kama una watoto, na unakaa maeneo haya ya Twin Cities, jiulize watoto hao wana fursa zipi za kupanua mawazo ili wawe raia wa dunia ya utandawazi wa leo. Unawaandaa vipi waweza kuwa na uzoefu wa kufanya kazi na kushirikiana na watu wa mataifa na tamaduni mbali mbali.

Ni wazi kuna vitu vikubwa ambavyo mzazi unaweza kufanya kwa lengo hilo. Lakini vile vile, kuna vitu kama haya matamasha ambayo yanachangia. Mimi kama mtafiti, mwalimu na mwandishi nahudhuria Afrifest kila mwaka. Napata fursa ya kufahamiana na watu, kukutana na wale ambao tunafahamiana, kuongelea shughuli zangu, na kuonesha vitabu na machapisho yangu mengine.

Kati ya vivutio vikubwa vya kesho ni kuwa Seneta Al Franken wa Minnesota atatembelea Afrifest yapata saa 10:30 alasiri hadi saa 11:00. Hiyo ni fursa ya nadra ya kuonana na mtu wa hadhi kama yake katika serikali ya Marekani.

Sunday, August 4, 2013

Mapendekezo ya Mwigulu Nchemba Kuhusu Ajira kwa Vijana

Jana, kwenye ukurasa wake wa Facebook, Mwigulu Nchemba ametoa mapendekezo kuhusu ajira, ambayo anasema atayawasilisha Bungeni kama hoja binafsi:

Habari vijana wenzangu, Nategemea kupeleka HOJA BINAFSI BUNGE LA 26 AUGUST 2013 KUHUSU AJIRA KWA VIJANA.

HINTS,
1) Kuitaka Serikali iitishe sensa ya wahitimu wote wa fani zote na ifanye uchambuzi wa ikama ya utumishi katika wizara, idara, mikoa, halmashauri- serikali za mitaa, na mashirika yake ya Umma. Lengo ni kujua idadi ya wahitimu wasio na kazi na nafasi zilizowazi. Utafiti wangu ni kwamba KWA UPANDE WA SERIKALI;

(A) KILA OFISI ya serikali INASHINDWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE ipasavyo KWA AJILI YA UPUNGUFU WA WATUMISHI, HAKUNA OFISI IMETIMIA WATUMISHI
(B) KUNA WATU WENGI SANA WANAKAIMU NAFASI MPK WENGENE WANAKAIMU NAFASI ZILIZOKUWA ZINAKAIMIWA yaani KAIMU KAIMU AFISA UTUMISHI NK NA NAFASI YAKE HIVYO HIZI NI tatu nafasi kwa mtu mmoja
(C) KUNA WATU wanapewa ajira za mikataba na WANAONGEZEWA MIKATABA KWA KIGEZO KUWA HAKUNA MTU ANAYEWEZA KUZIBA NAFASI HIYO au hakuna mwenye uzoefu.

KWA UPANDE WA PILI SASA WA WAHITIMU;

(1) KILA MTAA KUNA KIJANA AU VIJANA WAHITIMU WANA MIAKA 2 HADI 5 HAWANA KAZI WANAZUNGUKA NA BAHASHA MPAKA SOLI ZA VIATU ZINAKWENDA UPANDE
(2) KILA MTAA VIJANA WAPO WAKIOMBA KAZI WANAAMBIWA HAWANA UZOEFU wa 2 or 3 yrs, Au anayetakiwa awe na 4yrs experience hata katika ngazi za ofisa wa ngazi za kuanzia ilihali hakuna chuo kinafundisha uzoefu
(3) Vijana wapo na diploma hawajulikani walipo kwa Serikali na wamekaa miaka 2 hadi 5 na diploma zao wanasubiri kazi. kipindi ambacho angewezeshwa kwenda shule angeshavuka diploma na degree angekuwa hata na master.

Kufuatia hali hii
(i) vijana wanaitwa bomu ili hali VIJANA NI NGUVU KAZI YA TAIFA
(ii) Vijana wana stress, wamekata tamaa hawaoni future na wengine wanahasira sana
(iii) Vijana wahitimu wanatunzwa na wazee ambao hawakwenda shule hivyo kuwa mzigo kwa wazazi.

Lengo ni kuitaka serikali ikishajua idadi ya wahitimu na ikama yake cos ofisi ziko wazi mlioko ofisini mkisema ukweli msiogope mabosi wenu mtakiri hili

(1) Serikali ifanye re allocation ya vijana kwenye nafasi za kazi kufuatana na ujuzi wao,
(2) Serikali ianze kufanya attachment kwa vijana wapate uzoefu maofisini na hata kuwalipa half a saraly of a full employed officer ili kuondokana na tatizo la kukosa uzoefu kwa kijana aombapo kazi.
(3) Vijana wawe tayari kujitolea kulipwa hata half a saraly ili wapate uzoefu
(4) Uwezo wa kazi na marks za kwenye vyeti ni vitu viwili tofauti, serikali ikiwa attach ofisini vijana itajua uwezo wao itaacha kuongezea wastaafu mikataba kwa vigezo kuwa hakuna mwenye uwezo wa kuziba nafasi hiyo
(5) Serikali ibane matumizi yake ili itenge fedha ya kuendeleza wahitimu. Mtu mwenye diploma kusubiri kazi miaka 5 ni kipindi angeweza kuwa na degree na masters yake.
Baadhi sehemu za kukata matumizi ya serikali bila kuathiri kazi za serikali ni kwenye magari na mafuta ya magari. Unakuta bosi anakaa bunju halafu dreva gongolamboto halafu ofisi posta, au bosi kiluvya dreva mbagala ofisi posta kila siku trip hizo, pia training nje ya nchi kwa mtu mwenye 59yrs nakutumia milions and milions zisitishwe ili tuandae generetion ya kupokea majukumu.
Pia serikali ikishajua waliopo pia iandae projection ya tunakoelekea in three to five yrs hali itakuwaje na serikali inampango gani. Cos maisha bora yanaletwa na KAZI.
SERIKALI IKISHAJUA IWEKE BAJETI AMA YA GUARANTEE AU YA KUFUFUA VIWANDA VYOTE VILIVYO LABOUR INTENSIVE ili kuchukua vijana wahitimu na wa mtaani. SENSA HII SIO GHARAMA NI KUWATANGAZIA TU WAHITIMU WAKAJIANDIKISHE KTK OFC ILIOKARIBU AU KUPELEKA CV kwa DC the cv zinachambuliwa.

This is a rough idear. You can add or improve.

VIjanaaaaaaaa, itikieni NGUVU KAZI YA TAIFA

********************************************************************
Nami nimemjibu katika ukurasa huo huo wa Facebook kama ifuatavyo
:


Kwanza kabisa, andika ki-Swahili ipasavyo, sio kuchanganya na maneno ya ki-Ingereza, kama ufanyavyo. Tunapaswa kuonyesha kuwa tunaiheshimu lugha yetu. Kiswahili kinajitosheleza, sawa na lugha zingine. Lugha ni kioo cha nafsi na upekee wa jamii au taifa. Kuiheshimu lugha ni dalili ya kujiheshimu.

Hasa kwa mtu anayehesabiwa kuwa ni kiongozi, sherti kuonyesha mfano katika hili. Kama kiongozi unashindwa kuonyesha heshima kwa lugha yetu, unashindwa kuonyesha heshima wa utambulisho huu wa Taifa letu, ni kiongozi gani, na unawafundisha nini watoto wetu?

Ujumbe wako kuhusu ajira unapwaya sana. Hujaweka suala hili katika mkabala wowote, wala hujalifanyia utangulizi unaoonyesha kuwa unaelewa historia na upana wa suala hili. Hata dhana yenyewe ya ajira unayotumia ni finyu. Papo hapo unadai kuwa umefanya utafiti. Ni ajabu.

Hujazingatia tulikotoka, kwa Mwalimu Nyerere, ambaye aliongelea masuala haya ya ajira. Aliongelea masuala ya elimu kwa vijana, akisisitiza kuwa tuwape elimu ya kujitegemea. Inaonekana hujasoma lolote kuhusu mawazo ya Mwalimu Nyerere juu ya suala hili la elimu ya kujitegemea.

Ungefanya utafiti kuhusu kinchoendelea duniani, angalau ungegundua kuwa katika dunia ya leo, watu huongelea umuhimu wa kutoa elimu kwa vijana kwa lengo la kuwawezesha kujiajiri, kujitengenezea ajira.

Hilo hujataja, na haionekani unalifahamu. Wewe unaongelea ajira serikalini. Dhana hiyo, ingawa ilikuwa na mantiki kubwa miaka ya zamani, inapitwa na wakati. Na wewe kama kiongozi, ulipaswa utambue hilo, ili uweze kutoa ushauri mwafaka kwa hao vijana.

Unajiita kijana, lakini mawazo yako ni yale yaliyokuwa yanakubalika karne iliyopita, sio mawazo ya karne ya 21. Katika karne ya 21 kuwajengea vijana dhana kuwa waelekeze nguvu katika kutafuta ajira serikalini ni upotoshaji. Hii dhana kwamba Tanzania inahitaji viongozi vijana ni upuuzi, kama vijana wenyewe ni akina Mwigulu Nchemba. Hawafai kuongoza, kwa sababu hawajui dunia ikoje na inakwenda wapi.

Ingekuwa Mwigulu Nchemba unajua dunia ya leo ikoje na inakwenda wapi, kuhusu hili suala la ajira, ungefahamu kuwa sekta inayokuwa kwa kasi kuliko zote hapa duniani ni utalii. Hujataja jambo hilo, ambalo liko wazi miongoni mwa wote wanaofuatilia maendeleo ya uchumi na ajira katika karne hii.

Sekta ya utalii ndio inayokua kwa kasi kuliko zote, na ndio inayoleta matumaini ya kutoa ajira nyingi kuliko hiyo serikali ambayo ndio msingi wa mapendekezo yako.

Kama mtu unataka kutoa mchango katika suala la ajira kwa vijana, ni muhimu sana kuwafungua macho kuhusu sekta hii ya utalii, na jinsi ya wao kujiandaana kujipanga kunufaika na sekta hii.

Sisemi kuwa suala la ajira serikalini lisahauliwe. Lakini ninachosema ni kuwa tuwe na upeo mpana, upeo wa kuelewa hali halisi ya dunia ya leo. Tuwe pia watu ambao tumesoma yale aliyosema Mwalimu Nyerere kuhusu elimu ya kujitegemea.

Mwigulu ukiwa ni katibu mwenezi, nilitegemea unaeneza mawazo thabiti ya kuliendeleza Taifa. Lakini naona unaeneza mawazo rejareja, baadhi yakiwa yamepitwa na wakati. Mtu kama wewe hufai kuwa kiongozi. Wala usije ukadhani mimi ni CHADEMA. Mimi ni raia ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, ila nawashuhudia CCM mnavyojikanyaga.

Ninapenda kusema neno moja zaidi kuhusu Nyerere. CCM mmemsaliti Mwalimu Nyerere. Yeyote anayesoma "Azimio la Arusha" na maandishi mengine ataliona hilo. CCM ni chama kinachohujumu mapinduzi aliyoyawazia Mwalimu Nyerere.

Ungemsoma Mwalimu Nyerere, ungefahamu kuwa alikuwa anakazana sana kuleta mapinduzi vijinini, ili kuwe na fursa za kiuchumi na ajira, na hivi kupunguza ndoto ya vijana kuhamia mijini. Wewe andiko lako lote kuhusu ajira unawaelekeza vijana waende katika ajira za serikali. Ni kuwavutia waende mijini. Hujasema lolote kuhusu kuboresha maisha ya vijijini, uchumi wa vijijini, na ajira huko huko vijijini.

Kwa kumalizia, ningependa kujua iwapo Mwigulu Nchemba unasoma vitabu vyovyote. Ningependa kujua kama una vitabu nyumbani kwako. Ningependa kujua iwapo tangu mwaka huu uanze hadi leo, umesoma vitabu vingapi.

Saturday, August 3, 2013

Tundu Lissu: Pigeni Kelele Kuokoa Watanzania

Lissu: Pigeni kelele kuokoa Watanzania
Penulis : mtandao-net on Saturday, August 3, 2013 | 10:09 PM

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeutaka umoja wa vijana wa Vyama vya Kidemokrasia Duniani (IYDU) kupiga kelele kote duniani ili kuwanusuru Watanzania wanaouawa hovyo kwa sababu za tofauti za siasa hapa nchini.

Akizungumza na uongozi wa umoja huo (IYDU) jijini Dar es Salaam wiki hii, Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni Tundu Lissu alisema ni wakati wa vijana kuwaokoa wenzao wa Tanzania ambao kujiunga kwao na siasa kumesababisha wachukiwe na watawala.

“Watu wanauawa hadharani na hakuna hatua zinazochukuliwa…nendeni katika nchi zenu katika mabunge yenu mkapige kelele katika haya yanayotokea Tanzania; inaweza kusaidia na mkawa mmewasaidia Watanzania,” alisema Lissu. Tundu Lissu alisema viongozi wengi wamekamatwa na kufunguliwa kesi nyingi mahakamani, na hivyo kuifanya CHADEMA kuwa katika wakati mgumu kuliko mwingine wowote katika uendeshaji wa siasa za vyama vingi hapa nchini.

Chama hicho kimedai kuwa hali ya kisiasa hususan kwao na baadhi ya wapinzani nchini ni ngumu, kutokana na ukandamizaji mkubwa unaofanywa na serikali kwa kutumia vyombo vya dola.

Lissu alisema viongozi wa upinzani wamefunguliwa kesi za ugaidi kwa lengo la kuwafanya watumie muda mwingi katika kesi hizo, badala ya kuishughulikia serikali pale inaposhindwa kutimiza wajibu wake.

Mbali na kesi hizo, kumekuwa na matukio ya kikatili ya kuteka, kutesa na hata mauaji dhidi ya watu wanaoshabikia upinzani na wale wanaoikosoa serikali katika mambo ya msingi na yenye maslahi ya nchi.

Lissu amesema wabunge wa CHADEMA licha ya uchache wao, wakiwemo baadhi wa vyama vingine vya upinzani, wamejitahidi kupambana bila woga bungeni kutetea wananchi lakini wamekuwa wakizidiwa na wingi wa wenzao wa CCM, ambao wamekuwa wakipitisha maamuzi mengi ya hovyo na yasiyo na manufaa kwa nchi.

Mapema akiwaaga vijana hao, Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe, amewataka vijana kutokata tamaa kutokana na mambo yanayotokea nchini.

Mbowe alisema CHADEMA haitarudi nyuma katika harakati za kutwaa madaraka ya dola hata kama watawala waliopo madarakani hawapendelei nafasi zao kuwaponyoka.

“Tunafahamu katika siasa kuna magumu mengi lakini niwahakikishieni kuwa ninyi mna nafasi kubwa ya kuleta mageuzi sehemu yoyote kama mtakuwa na dhamira na kuvishinda vitisho mbali mbali dhidi yenu,” alisema Mbowe.

Katika ziara yao hapa nchini vijana hao wa IYDU walitembelea ofisi mbali mbali ikiwamo Wizara ya Mambo ya Nje na ubalozi wa nchi za Ulaya nchini (EU).

Mkurugenzi wa masuala ya Mashariki ya Mbali, Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Simba Yahya, alikiri kuwa watumishi wa umma wanashindwa kutofautisha utendaji wa serikali na chama kilichoko madarakani.

“Itachukua muda kwa wafanyakazi kutenganisha hali hii….. kiuhalisi wanatakiwa wawe watendaji kwani wapinzani wa leo wa serikali ndio wanaweza kuwa mabosi wao wa kesho,” alisema Yahya.

Sunday, July 28, 2013

Wageni Kutoka Tanzania


Wiki hii nimekuwa na bahati hapa Minnesota ya kukutana na wageni wawili kutoka Tanzania. Mgeni wa kwanza, Ndugu Charles Mpanda kutoka Arusha, tulionana tarehe 25 mjini Rochester, tukapiga picha inayoonekana hapa kushoto. Habari ya tukio hili niliandika hapa. Nitaandika zaidi katika blogu hii ya "hapakwetu."










Leo nimeenda mjini New Prague, kuonana na mgeni mwingine, Fr. Setonga, ambaye naonekana naye katika hiyo picha ya chini. Fr. Setonga tumewasiliana kwa miaka mingi kidogo, kwa simu na barua pepe, ila hatukuwahi kuonana. Leo imekuwa bahati ya kuonana.

Tumeongelea masuala mbali mbali, kuhusu dini yetu, kuhusu juhudi na mafanikio ya Kanisa Katoliki katika sekta ya elimu, sehemu mbali mbali duniani, kwa karne hadi karne, kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu. Hii inatokana na msimamo wa Kanisa Katoliki wa kuthamini sana elimu. Kwangu mimi niliyesomeshwa katika shule za Kanisa Katoliki, ni jambo la kujivunia na kushukuru kwamba walinifundisha maadili na nidhamu ya kazi ya kiwango cha juu kabisa, pamoja na kuzingatia vipaji na uwezo tunapata kutoka kwa Mungu, na kwa ajili ya kuwahudumia wengine.

Tuligusia mfano hai wa jinsi Kanisa Katoliki linavyokazana kufungua matawi ya chuo kikuu cha Mtakatifu Augustin nchini Tanzania. Nilimdokezea Fr. Setonga kuwa ninawazia kwenda kufundisha katika chuo hiki, kama njia moja ya kutoa shukrani kwa Kanisa.

Kati ya mambo mengine tuliyoongelea kwa undani, tukakubaliana, ni umuhimu wa sisi waumini wa Tanzania kuwa wafadhili wa kanisa letu na shughuli zake mbali mbali. Itakuwa ni faraja na jambo la kujivunia iwapo tutabeba majukumu ambayo aghalabu yamebebwa na wafadhili kutoka nchi za nje, hasa Ulaya na Marekani.

Friday, July 26, 2013

Mwaliko Mkutanoni Finland

Nimepata mwaliko kwenda kushiriki mkutano wa wanataaluma Finland, katika chuo kikuu cha Turku. Mkutano ufanyika kuanzia tarehe 19 hadi 24 Agosti na mada yake itakuwa The Role of Theory in Folkloristics and Comparative Religion." Nitakuwa mmoja wa watoa mada wateule, na mhadhara wangu utahusu "The Epic as Discourse on National Identity," kama ilivyotajwa katika programu hii hapa.

Mkutano huu wa wanataaluma umeandaliwa kwa kumbukumbu ya marehemu Profesa Lauri Honko, mmoja wa wataalam wakubwa kabisa duniani katika. Wa-Tanzania labda watafurahi kusikia kuwa Profesa Honko alifanya utafiti sehemu mbali mbali za dunia, ikiwemo Tanzania. Niliwahi kumwona,  na kuwa naye kwa wiki kama mbili hivi, wakati nilipohudhuria warsha ya watafiti ambayo aliiendesha Turku mwaka 1991. Alikuwa ni mtaalam sana, aliyekuwa anaongea kwa kujiamini kabisa, lakini mtu mtaratibu na mpole. Ukisoma vitabu vyake na makala zake, unaona wazi kabisa kuwa alikuwa mwenye mawazo mazito yenye kutoa mchango mkubwa kwa taaluma.

Kati ya mambo mengi aliyofanya, ikiwa ni pamoja na kuandika vitabu na makala na kutoa mihadhara, Profesa Honko aliisaidia UNESCO kwa kuandaa sera ya kuhifadhi utamaduni.

Sio jambo geni kwangu kupata mialiko ya aina hii. Najisikia raha kwenda kuuelezea ulimwengu fikra, mitazamo, na matokeo ya utafiti wangu. Papo hapo ni fursa ya kukutana na wataalam wengine na kubadilishana mawazo na uzoefu. Ndivyo taaluma inavyokua na kustawi.

Hata hivi, sitakuwa na raha sana kwenye mkutano huu wa Turku, kwani nitakuwa namkumbuka Profesa Honko.  Ni jambo jema kwamba mkutano utakuwa ni kwa kumkumbuka, lakinii papo hapo masikitiko ya kutokuwa naye yatakuwepo. Mungu amweke mahali pema Peponi.

Thursday, July 18, 2013

Kiu ya Kusoma Vitabu

Daima nina kiu ya kusoma vitabu.  Sio rahisi unikute sina kitabu. Hii sio tu kwa vile mimi ni mwalimu. Ni tabia ambayo nilijengeka nayo tangu nikiwa kijana mdogo.

Kuwa mwalimu kumenipa motisha zaidi ya kusoma sana vitabu. Wakati huu ninapoandika, wanafunzi wangu na mimi tumemaliza kusoma Half of a Yellow Sun kilichoandikwa na Chimamanda Ngozi Adichie. Sote tumekifurahia sana. Lakini, mwandishi huyu amechapisha hivi karibuni na kitabu kingine kiitwacho Americanah, ambacho tayari kinazungumziwa sana miongoni mwa wapenda vitabu. Kwa hivi, nami najipanga kujipatia kitabu hiki, nikisome.

Kitabu kingine ambacho tumekimaliza katika darasa tofauti siku chache zilizopita ni Midnight's Children cha Salman Rushdie.  Kitabu hiki ni kama chemsha bongo, kwa jinsi kilivyotumia mbinu mbali mbali za kuelezea maisha ya mhusika mkuu Saleem Sinai. Maisha hayo yamefungamana na historia ya India, tangu dakika ile India ilipopata uhuru, usiku wa manane, mwaka 1947. Rushdie amechanganya matukio ya historia na ubunifu wake wa ajabu katika kitabu hiki.

Midnight's Children ni kitabu kinachokutegemea msomaji uwe na ufahamu fulani wa mila, desturi na dini za India, hasa u-Hindu, u-Islam, u-Kristu, na u-Parsi. Uwe na ufahamu fulani wa historia ya India hasa katika karne ya ishirini, inayojumlisha viongozi maarufu kama Mahatma Gandhi, Jawaharlal Nehru, Muhammad Ali Jinnah, na Indira Gandhi. Ujue mazingira yaliysababisha kuzaliwa kwa nchi mbili za India na Pakistan, na mgogoro wa Kashmir, ambao bado unaendelea. Kwa bahati nzuri, katika miaka niliyofundisha hapa chuoni St. Olaf, nimefundisha sana fasihi ya India na hayo yote niliyoyataja.

Tulipofikia ukurasa wa mwisho wa kitabu hiki, tulijisikia kama washindi wa mashindano magumu. Kwa upande wangu, baada ya kupambana na Midnight's Children hadi mwisho, nimejawa na hamasa ya kusoma kitabu kingine cha Rushdie Satanic Verses, ambacho nilikinunua zamani, nikajaribu kukisoma, bila kufika mbali. Ninahisi kuwa kwa kusoma Midnight's Children nimejiandaa vilivyo kukabiliana na Satanic Verses. Au labda nianzie na kitabu chake kiitwacho The Enchantress of Florence, ambacho nimekuwa nacho kwa miaka kadhaa, bila kukisoma.

Ni jambo jema kujaribu kusoma maandishi mbali mbali ya mwandishi yeyote, sio kitabu kimoja tu. Kwa mfano, kwa upande wa Tanzania, utawakuta watu wakitaja kitabu cha Hamza Njozi kuhusu mauaji ya Mwembechai lakini hawajui kuwa mwandishi huyu amechapisha vitabu vingine pia, na makala nyingi, kuhusu u-Islam na fasihi.

Vile vile, wengi wakisikia jina la Salman Rushdie, wanalihusisha na kitabu cha Satanic Verses tu. Huu nao ni uzembe, kwani mwandishi huyu amechapisha vitabu vingi, kuanzia riwaya hadi insha kuhusu masuala mbali mbali ya sanaa, siasa na utamaduni. Kumtendea haki Rushdie ni lazima tusome maandishi yake mbali mbali.

Akili zetu zinapaswa ziwe na duku duku isiyoisha ya kujua mambo. Njia moja kuu ya kujaribu kukidhi kiu hii ni kusoma sana vitabu. Hapo utaona kwamba, tofauti na imani ya jamii yetu ya Tanzania, wajibu wa kusoma vitabu ni wa watu wote, sio wanafunzi tu.

Wednesday, July 17, 2013

Chezea Arusha Weye

Katuni hii imenipendeza. Sina zaidi, bali niseme tu haka kajibwa kanatisha. Tena usiombee kukutana nako.

Ingawa mchoraji hajataja mambo ya uchaguzi wa madiwani uliofanyika siku chache zilizopita, katuni inayapeleka mawazo yetu kwenye uchaguzi huo, ambao matokeo yake yamekuwa CHADEMA kushinda kata zote nne zilizokuwa zinashindaniwa.

Matokeo hayo hayakunishangaza. Kwa miaka kadhaa, katika pitapita zangu Arusha, nikiongea na madereva wa teksi, mafundi viatu, na wauza mitumba, nimejionea nguvu za CHADEMA katika mji ule. Nilithubutu hata kuandika makala kuhusu nguvu ya CHADEMA mjini Arusha. Makala hiyo ni hii hapa. Niliandika hayo, na leo ninaandika tena, ingawa mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa.

Thursday, July 11, 2013

Tumeanza Kusoma "Abyssinian Chronicles"

Baada ya kumaliza kitabu cha Half of a Yellow Sun, darasa langu la fasihi ya Afrika tumekuwa tukisoma Abyssinian Chronicles, riwaya ya Moses Isegawa.

Moses Isegawa ni kijana aliyezaliwa na kukulia Uganda. Lakini mwaka 1990 aliondoka Uganda akaenda kuishi Netherlands, akiwa amechukua uraia wa nchi ile.

Nilikuwa nimesikia habari za kitabu chake hiki kwa miaka kadhaa. Nilinunua nakala, ila sikupata fursa ya kukisoma, ingawa nilikipitia juu juu. Hata hivyo katika kukipitia hivyo, niliona wazi kabisa kuwa ni kitabu murua, kilichoelezea kwa ufasaha na mvuto mkubwa maisha ya leo ya watu wa Uganda, kuanzia kijijini hadi mjini.

Nilipokuwa naandaa kozi yangu hii, miezi michache iliyopita, niliamua kitabu hiki kiwemo katika orodha yangu. Tumesoma karibu kurasa 100 tu,  wakati kitabu kina kurasa 480. Kiasi tulichosoma kimetupa fursa ya kuongelea dhamira mbali mbali zinazojitokeza, kama vile mila na desturi za arusi, masuala ya wahusika, na sanaa.

Kwa upande wangu, nimekuwa nikiwaambia wanafunzi kuwa maelezo ya maisha ya vijijini yamenikumbusha maisha yangu mwenyewe, maana nilizaliwa na kukulia nilikulia kijijini.

Moses Isegawa alikiandika kitabu hiki kwa lugha ya kidachi (Dutch), na jina lake lilikuwa Abessijnse kronieken, ambacho kilichapishwa Amsterdam mwaka 1998. Nakala 100,000 ziliuzwa hima, ingawa idadi ya watu wa nchi ile ni yapata milioni 16 tu.

Mwandishi alikiweka kitabu chake hiki katika lugha ya ki-Ingereza. Kwa kawaida, tunasema alikitafsiri. Lakini kwa mujibu wa falsafa za leo, dhana ya tafsiri ni dhana tata, na kile tunachokiita tafsiri sio tafsiri kwa kweli, bali utungo mpya. Huo ndio mtazamo wangu kuhusu Abyssinian Chronicles.

Muhula wetu umeisha leo, na mategemeo yangu ni kuwa wanafunzi na mimi mwenyewe tutaendelea kukisoma kitabu hiki hadi ukurasa wa mwisho. Sioni kama kuna tatizo kufikia mwisho wa muhula bila kumaliza kusoma kitabu. Dhana ya kumaliza kusoma kitabu nayo ni dhana tata na naweza kusema ni dhana muflisi. Kwa kutafakari kwa undani maana ya kusoma ni nini, na nini kinafanyika tunaposema tunasoma kitabu, nimejionea kuwa huwezi kumaliza kusoma kitabu chochote, hata kama umefika ukurasa wa mwisho na sentensi ya mwisho. Hilo ni suala jingine la falsafa, ambalo nalifafanua wakati wa kufundisha fasihi.

Abyssinian Chronicles ni kitabu kinachoelezea mambo ya miaka ya karibuni, ya sabini na kitu hadi themanini na kitu. Kinavutia sana. Ni ushahidi mwingine wa jinsi wenzetu wa nchi jirani, na wa nchi zingine za Afrika, walivyo katika anga za juu sana katika uandishi kwa lugha hizi za kigeni.

Wednesday, July 10, 2013

Taasisi ya Sir Emeka Offor Yachangia Vitabu

Sir Emeka Offor Foundation of Nigeria donates $600,000 to St. Paul-based Books for Africa; Largest donation ever

E-mail Print PDF
books for africa photo-3238792 orig
Books for Africa photo
The Nigeria-based Sir Emeka Offor Foundation has donated $600,000 to Books For Africa (BFA), which will support the shipment of more than a million books to the children of Nigeria and across Africa.

"This donation represents the largest single donation we have ever received at Books For Africa, so naturally we are quite excited," said Patrick Plonski, executive director of BFA. "The generosity of Sir Emeka Offor in advancing education across the African continent is an outstanding example for others to follow."

Tom Warth, who founded BFA in 1988, said that the "benefits that will accrue to the young people of Africa through this generous donation are immeasurable. We at Books For Africa struggle every day to convince folks of the wisdom of education in the advancement of African nations. Over our 25 years many have agreed with us but to have your generous donation as an example in the future will make our task easier."

In a unique partnership with BFA that began in 2010, the Sir Emeka Offor Foundation has agreed to sponsor major shipments of books to Nigeria and The Gambia. In 2010, the Foundation sponsored eight containers to students in Nigeria and in 2011, another 16 containers, a total of about 530,000 books.

In 2012, the foundation sponsored the shipment 110,000 books for school children as part of Books For Africa's "Million Books to The Gambia" campaign.

The $600,000 donation will support the shipment of an additional one million books to the children of Africa. With funding provided by this grant, planning is currently under way to distribute an additional 1.1 million books to Nigeria, the Gambia, Somalia, Liberia, Tanzania, Namibia, Senegal, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Botswana, South Africa, sierra Leone, Malawi and Egypt.

The Sir Emeka Offor Foundation is a non-governmental philanthropic organization whose founder, Sir Emeka C. Offor, began in the 1990s to positively render assistance to the needy in society in various ramifications irrespective of tribe, creed, religion and nation.

Books For Africa is the world's largest shipper of donated text and library books to the African continent. It has shipped over 28 million books to 49 African countries over the past 25 years.

CHANZO: InsightNews.com

Thursday, July 4, 2013

Tumemaliza Kusoma "Half of a Yellow Sun"

Kwa wiki hizi sita, katika kipindi hiki cha "summer," nimekuwa nikifundisha kozi juu ya fasihi ya Afrika. Jana tumemaliza kusoma Half of a Yellow Sun, riwaya ya Chimamanda Ngozi Adichie wa Nigeria.  Huyu ni mwandishi chipukizi, lakini tayari ameshajipatia umaarufu sana na nyota yake inazidi kung'ara.

Amechapisha vitabu kadhaa akianzia na Purple Hibiscus na The Thing Around Your Neck. Ninavyo vitabu hivyo, na nimeshawahi kufundisha Purple Hibiscus.  Hivi karibuni, amechapisha Americanah, kitabu ambacho kinaongelewa sana miongoni mwa wasomaji, walimu, na wahakiki.

Kilipochapishwa kitabu cha Half of a Yellow Sun, nilisoma taarifa zake. Taarifa hizi zilielezea kuwa kitabu hiki kinahusu vita ya wenyewe kwa wenyewe nchini Nigeria, ambapo sehemu ya kusini mashariki ilijitenga na kutangaza kuwa imekuwa taifa huru la Biafra.

Mwaka 2008 Chimamanda Ngozi Adichie alikuwa mmoja wa waandishi walioalikwa kuhudhuria tamasha la vitabu Minneapolis. Alikuja kuzindua kitabu cha Half of a Yellow Sun. Nilihudhuria, nikasikiliza hotuba yake, kisha nikajumuika na umati wa watu waliokuwa wananunua nakala na kusainiwa na mwandishi. Nilipata pia fursa ya kupiga naye picha inayoonekana hapa kushoto.

Pamoja na kuwa nilinunua nakala ya Half of a Yellow Sun siku hiyo, sikupata fursa ya kukisoma. Lakini miaka yote hii nilikuwa na nia ya kufanya hivyo, na nimefanya hivyo katika kufundisha somo la fasihi ya Afrika.

Wote tumependezwa sana na Half of a Yellow Sun. Chimamanda Ngozi Adichie ana kipaji kikubwa sana cha kubuni na kusimulia hadithi. Yeyote anayesoma maandishi yake na anakijua ki-Ingereza vizuri, atakiri kuwa mwandishi huyu anaimudu vizuri sana lugha hiyo. Ni kweli kuwa kwa ujumla Half of a Yellow Sun inahusu vita ya Biafra, 1966-1970, lakini kwanza inaongelea maisha ya kila siku ya watu, hasa katika mazingira ya Chuo Kikuu cha Nsukka. Chimamanda alizaliwa na kukulia hapo, na katika maandishi yake hupenda kuongelea maisha ya wasomi na familia zao chuoni pale.

Hata katika mazingira ya vita, Half of a Yellow Sun inatuonyesha watu wakijitahidi kuendelea na shughuli zao za kawaida, kama vile kuelimisha watoto, hata kama ni chini ya mti. Tunawaona watu wakitafuta riziki za maisha. Na tunawaona watoto wakicheza michezo, pamoja na dhiki kubwa ya magonjwa na njaa. Pamoja na ukatili mkubwa uliojitokeza katika vita ya Biafra, Chimamanda Ngozi Adichie amejiepusha na kishawishi cha kuangalia suala zima kama suala la aina mbili tu ya watu, yaani wabaya na wema. Anaonyesha jinsi binadamu tulivyo na uwezo wa kuwa wabaya, sawa na wale ambao tunawaona ndio wabaya.

Half of a Yellow Sun imefuata vizuri mtiririko wa matukio yaliyotangulia vita na matukio ya vita yenyewe. Kwangu mimi kama m-Tanzania, nimeguswa na jinsi Chimamanda Ngozi Adichie alivyoelezea mchango wa Tanzania katika kuiunga mkono Biafra. Ameelezea furaha ya watu wa Biafra na heshima waliyokuwa nayo kwa Tanzania na Mwalimu Nyerere. Wakati nasoma kitabu hiki na suala hili la Tanzania, nilikumbuka kitabu kipya cha Chinua Achebe kiitwacho There Was a Country. Humo Achebe ameelezea vizuri sana jinsi msimamo wa Tanzania ulivyoshangiliwa na watu wa Biafra. Jina la Tanzania lilikuwa linatajwa kila mahali. Miziki ya Tanzania ilipigwa kila mahali. Katika Half of a Yellow Sun, kuna baa ambayo ilibadilishwa jina ikaitwa Tanzania Bar.

Kwa wasiofahamu napenda kusema kuwa sehemu iliyoitwa Biafra ni sehemu wanayoishi zaidi watu wa kabila la Igbo. Kutokana na siasa za Nigeria, ambamo ukabila una nafasi kubwa sana, dhuluma dhidi ya waIgbo, ikiwemo wengi kuuawa, hasa sehemu za kaskazini mwa Nigeria, ndio kitu kilichosababisha wakakimbilia kwao na kujitangaza kuwa ni taifa huru la Biafra. Chinua Achebe, ambaye alifariki hivi karibuni, na Chimamanda Ngozi Adichie ni wa kabila hilo.

Kwa kumalizia, bora niseme tu kwamba kuliko kusimuliwa, ni bora mtu ujipatie nakala ujisomee. Nasema hivyo nikijua fika kwamba ushauri huu hauna maana kwa jamii ya wa-Tanzania, kwani utamaduni wa kununua vitabu na kuvisoma haupo. Kuna uwezekano mkubwa kwamba ushauri wangu utazingatiwa na watu wa nchi zingine kama vile Kenya, ambayo ni makini kwa masuala ya aina hiyo.

Monday, July 1, 2013

Makala ya "New York Times" Yaongelea Udhalimu Tanzania

Nicholas Kulish wa gazeti la New York Times amechapisha makala kuhusu vitendo viovu ambavyo vimekuwa vikifanyika Tanzania, vitendo ambavyo ni ukiukwaji wa haki za binadamu. Isome makala hiyo hapa

Thursday, June 27, 2013

Mganga wa Kienyeji Akamatwa Akijaribu Kuloga Ndani ya Mahakama Kisutu


MGANGA WA KIENYEJI AKAMWATA AKIJARIBU KULOGA NDANI YA MAHAMAKA YA HAKIMU MKAZI KISUTU LEO






MGANGA WA KIENYEJI HUYU HAPA PICHANI, RAJABU ZUBERI(30),MKAZI WA Kerege,Muheza Tanga, akiwa chini ya ulinzi wa wanausalama leo saa mbili asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, baada kifaa maalum cha upekezi kumnasa mganga huyo akiwa na vifaa hivyo vya uganga ambavyo alikuwa amekuja navyo mahakamani hapo kwaajili ya kufanyia mambo ya kishirikina katika kesi moja inayomkabili 
mmoja wa washtakiwa mahakamani hapo. Hongereni sana wanausalama kwa kazi nzuri ya kumnasa mtu huyo kwani mmesaidia kuvuruga azma yake.Picha kwa hisani ya Happy Katabazi

CHANZO: Jamii Forums


Wednesday, June 26, 2013

Waraka kwa Rais Obama Kutoka kwa Kamati ya Ulinzi wa Wanahabari

Powered by Translate

The Committee to Protect Journalists writes to President @BarackObama ahead of his meeting with President @jmkikwete


The Committee to Protect Journalists wrote to U.S. President Barack Obama ahead of his meetings with Tanzanian President Jakaya Kikwete next week to ask that he bring up the critical importance of press freedom to economic development and democracy.
cpj_logo
June 25, 2013
His Excellency Barack Obama
President of the United States of America
White House
Via facsimile: +1 202-456-2461
Dear President Obama:
Ahead of your first trip to East Africa, we would like to bring to your attention the deteriorating state of press freedom in Tanzania. In your meetings with Tanzanian President Jakaya Kikwete, we ask that you discuss the critical importance of press freedom to economic development and democracy.
In the past year, CPJ has documented a rise in threats and attacks against journalists in Tanzania. In September 2012, CPJ documented the first work-related journalist killing in the country since we began keeping detailed records in 1992. Police shot at point-blank range Daudi Mwangosi, reporter for TV Channel 10, after the journalist confronted them over the arrest of another reporter. A junior officer was arrested, but several other officers seen as being involved have not been held accountable. Another journalist, Issa Ngumba, was found dead from gunshot wounds in January. CPJ is investigating to determine if the murder was related to his coverage of local farming issues. No one has been arrested.
In addition, several journalists have been attacked in connection with their work. In March, unknown assailants attacked Absalom Kibanda, chairman of Tanzanian Editor's Forum and managing editor of the New Habari media company, leaving the critical columnist with severe injuries. No one has been arrested. Local journalists also said they have often been threatened by officials and high-ranking businessmen via text messages, emails, or intermediaries. Reporters based outside the capital, Dar es Salaam, are often targeted, the sources said.
This new trend of attacks against the press in Tanzania occurs against a backdrop of restrictive anti-press laws. One of them, the 1976 Newspaper Act, which allows the information minister discretionary powers to suspend publications, was used to ban the leading independent weekly Mwanahalisi in July 2012. The constitution includes at least 16 other anti-press laws that have induced journalists to practice self-censorship, our research shows.
Tanzanian authorities said they would present a new press bill this year that would eliminate legislation that censors or restricts the press. But the contents of the bill have been kept from the public, and local and regional media outlets have said they fear renewed anti-press legislation.
As you know, the Tanzanian government is one of five African nations that signed on to your Open Government Partnership Initiative, a multilateral effort to promote transparency. Tanzania cannot uphold its obligation given the current media climate of threats against the press and existing restrictive legislation. Economic development that benefits Tanzanian citizens can only occur in a system in which officials are held accountable by a free and vibrant press.
Tanzanian journalists are working in a highly restrictive media environment and are being attacked with impunity. We ask that you urge President Kikwete to promote media freedom in the country, without which vibrant democracy and economic development cannot exist.
Sincerely,
Joel Simon
Executive Director
CC List:
H.E. Jakaya Kikwete, President of Tanzania
H.E. Mwanaidi S. Maajar, Ambassador of Tanzania to the United States of America
H.E. Alfonso E. Lenhardt, Ambassador of the United States of America to the Republic of Tanzania
Filiberto Ceriani Sebregondi, Head of the Delegation of European Union to the Republic of Tanzania
John Kerry, Secretary of State for the United States of America
Linda Thomas-Greenfield, Assistant Secretary for African Affairs for the United States of America
Dr. Fenella Mukandara, Minister of Information of the Republic of Tanzania
Pansy Tlakula, Special Rapporteur on Freedom of Expression and Access to Information, African Commission on Human and Peoples' Rights
Reginald Mengi, Chairman of the Media Association of Tanzania
Dr. Jeffrey Ashley, USAID / East Africa Mission Director
Kajubi Mukajanga, Executive Secretary of the Media Council of Tanzania
Mohamed Tibanyendera, Chairman of the Media Institute of Southern Africa, Tanzania
Ernest Sungura, Executive Director of the Tanzania Media Fund

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...