Warsha Kuhusu Utamaduni na Utandawazi, Juni 12, 2010
Hebu fikiria: hao wa-Tanzania wanaoondoka nchini kwenda kufanya kazi nchi za mbali au kutafuta biashara, kusoma, na kadhalika, wanakuwa wamejiandaa vipi kukabiliana na tamaduni za huko wanakoenda? Wageni wanaokuja Tanzania kwa shughuli mbali mbali, au kama wahamiaji, nao wanakuwa wamejiandaa vipi kuishi katika utamaduni wetu? Masuala ya aina hii yameanza kupata umuhimu wa pekee duniani, kutokana na kuimarika kwa utandawazi. Ni aina ya masuala ambayo ninayashughulikia sana, kama mwandishi, mtoa mada na mwendesha warsha, hasa huku Marekani. Ni muhimu wa-Tanzania nao wajipange na kujiandaa ipasavyo, kwani kama ninavyosema mara kwa mara katika blogu hii, ushindani unaendelea kushamiri duniani, na uwezo wa kukabiliana na ushindani huu unatokana na elimu, ujuzi na maarifa. Tarehe 12 Juni nitaendesha warsha Tanga, kuhusu utamaduni, utandawazi, na maendeleo. Nimeshaendesha warsha za aina hii kabla hapa Tanzania. Yeyote anakaribishwa. Kwa taarifa zaidi kuhusu warsha ya tarehe 12 Juni, som