Sunday, June 27, 2021

Kitendea Kazi


Hii picha ya kitabu changu imetoka kwa Abraham Thomas aishiye Mto wa Mbu, Tanzania. Ni kitabu ambacho yeye na wenzake wamekuwa wakikitumia katika shughuli za kuongoza watalii na katika mazingira mengine.

Ukiona jembe limechakaa, ujue linatumika. Kitabu hiki ni sawa na jembe. Mashuhuda ni waMarekani wenye shughuli yoyote na waAfrika, pia waAfrika kama Abraham Thomas wenye shughhuli yoyote na waMarekani. Kinaepusha migogoro na kuchangia ufanisi.

Wednesday, June 23, 2021

KITABU KINAPATIKANA ARUSHA

Mjasiriamali wa Arusha anauza kitabu hiki ambacho kimekuwa gumzo huku nje ya Tanzania hadi hivi karibuni katika Trade With Africa Business Summit, mkutano uliohudhuriwa na watu maarufu kutoka nchi mbali kuanzia Umoja wa Afrika, hadi Israel, Ujerumani, Nigeria, Ghana, Afrika Kusini, na Marekani. Piga simu namba 0787 597 202

Sunday, June 13, 2021

Hitimisho la Trade with Africa Business Summit 2021

Video hii ni ya hitimisho la mkutano uliofanyika tangu Mei 31 hadi Juni 4, uitwao "Trade With Africa Business Summit." Nimeshautajataja mkutano huu hapa. Kila mtu alishukuru kwa kuhudhiria kutokana na elimu kubwa na pana iliyopatikana katika mihadhara na mijadala.

Mwaandaaji wa mkutano, Toyin Umesiri, alikuwa amenialika nikaongelee kitabu changu, "Africans and Americans: Embracing Cultural Differences." Kitabu kilitajwatajwa kwenye mkutano, hata katika video hii ya dakika za mwisho za mkutano. Mtoa mada Vera Moore, mmiliki wa kampuni ya Vera More Cosmetics, anaonekana mwishoni kabisa akiwa ameshika kitabu. Tulishangaa amekipataje upesi namna ile.

Namshukuru Toyin kwa mwaliko wake. Ameniarifu kuwa ataendelea kunibebesha majukumu, nami niko tayari. Video zote za mkutano zinapatikana mtandaoni. Nikizingatia thamani ya elimu iliyomo, kulipia gharama iliyotajwa ni sawa na uwekezaji makini. Zinapatikana hapa: https://www.nazaru.trade/courses/5248326/content

Thursday, June 10, 2021

Nina Wasomaji Butiama kwa Mwalimu Nyerere

Sijawahi kufika Mwitongo, Butiama, lakini kitabu changu, ambacho ni kama nafsi yangu, kimefika. Pichani anaonekana mjukuu wa Mwalimu Nyerere akiwa anasoma kitabu hiki. Picha hii aliiweka mitandaoni akiwa ameambatisha ujumbe. Ninanukuu baadhi ya aliyosema.

"My Dad gave me this book to read this morning, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences by Joseph Mbele. I just finished it. One lesson I learned is to respect, understand, and see the value in both cultures. I would highly recommend this book." .................. "My Dad gave me this book, he felt that it could be helpful for me, I’ve lived in the US since I was 7, I’ve made the decision to move back this year. There are many things which I still question. It will be a long learning process, this book has given me hope." .................. "Thank you for writing this book Professor Mbele. I’ve learned quite a lot from reading it but I’ve also grasped a better understanding of many things which haven’t been clear to me before."

Naleta tafsiri yangu kwa kiSwahili:

"Baba alinipa kitabu hiki asubuhi hii nisome, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, cha Joseph Mbele. Nimemaliza sasa hivi. Jambo moja ambalo nimejifunza ni kuheshimu, kuelewa, na kuona thamani ya tamaduni zote mbili. Ninanipendekeza sana kitabu hiki."....

" Baba alinipa kitabu hiki, kwa kuona kwamba kingeweza kunisaidia. Nimeishi Marekani tangu nikiwa na miaka saba, na nimeamua kurejea nyumani mwaka huu. Kuna mambo mengi ambayo bado nayahoji. Itanichukua muda mrefu kujifunza; kitabu hiki kimenipa matumaini."....

"Asante kwa kuandika kitabu hiki Profesa Mbele. Nimmejifunza mengi kwa kukisoma na nimepata uelewa mzuri wa mambo mengi ambayo hayakuwa wazi kwangu."

Saturday, June 5, 2021

Ms. Vera Moore - Mdau Mpya wa Kitabu Changu

Wiki hii nzima, nimekuwa nikihudhuria mkutano mkuu uitwao Trade With Africa Business Summit. Mkutano umejumlisha wafanya biashara, wanadiplomasia, na wajasiriamali, na wengine kutoka nchi mbali mbali. Mwandaaji wa mkutano, Toyin Umesiri kutoka Nigeria, mjasiriamali na mhamasishaji wa biashara baina ya Afrika na Marekani, alikuwa amenialika kuongelea kitabu changu, "Africans and Americans: Embracing Cultural Differences." Alikipigia debe mkutanoni, na kilitajwa mara kwa mara. Mjumbe mmoja, Vera Moore, mfanyabiashara maarufu wa vipodozi, alitusisimua alipokuwa akiongea, kwa kutuonyesha nakala ya kitabu akisema ameshanunua. Nilishangaa alivyokinunua haraka namna ile. Nafurahi kuwa na mdau maarufu huyu. Wengine wanakuja.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...