Monday, March 24, 2014

Namshukuru Mungu kwa Kunitoa Hospitalini

Tangu tarehe 1 Februari hadi tarehe 20 Machi nililazwa katika hospitali ya Allina Northwestern Minneapolis. Sasa niko nyumbani chini ya usimamizi wa wataalam wa kuimarisha afya ya viungo. Namshukuru Mungu.

Nawashukuru ndugu, jamaa, marafiki kutoka sehemu mbali mbali za dunia kwa salamu na sala zao. Nawashukuru madaktari na wauguzi. Inavyoonekana, nitakuwepo tena mitaani baada ya wiki kadhaa, Insha'Allah.


Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...