Tamko la CHADEMA Kuhusu Migomo na Maandamano ya Amani

TAMKO LA CHAMA JUU YA UTEKELEZAJI WA AZIMIO LA MKUTANO MKUU KUHUSU MIGOMO NA MAANDAMANO YA AMANI NCHI NZIMA Ndugu waandishi wa habari Tunapenda kuanza mkutano huu kwa kutoa salaam za amani kwa Watanzania wote, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Amani Kimataifa, ambayo huadhimiswa Septemba 21, ya kila mwaka. Kauli mbiu ya mwaka huu kama ilivyotolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon ni ‘The Right Of People’s to Peace’. Tumekutana nanyi hapa siku hii mahsusi ya kuazimisha amani kimataifa, tukiwa na ujumbe maalum kwa Watanzania kuwaeleza namna ambavyo watawala wa Serikali ya CCM, wanavyohatarisha amani ya nchi yetu kwa kuvunja haki za msingi za Watanzania huku pia wakififisha matumaini ya wananchi. Tunataja maneno hayo mawili HAKI na MATUMAINI kwa makusudi kabisa kwa sababu hayo ndiyo ndiyo msingi wa amani na utulivu wa kweli mahali katika taifa ambalo linajali na kuzingatia maendeleo na ustawi wa wananchi wake. Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere katika moja