Sunday, November 29, 2020

Hata Balozi wa Japani Kalalamikia Uchaguzi wa Tanzania

Ule unaoitwa uchaguzi ambao ulifanyika Tanzania tarehe 28 mwezi Oktoba umelalamikiwa sana ndani na nje ya nchi. Kilichonishtua zaidi ni kuwa hata Balozi wa Japani nchini Tanzania amelalamika, kwa tamko hili:
I am troubled by the information of widespread irregularities and wrongdoings during the recent election process in this country. I am convinced that sound democracy based upon multiparty system works best to contribute to further development and prosperity of Tanzania.
(GOTO Shinichi, Ambassador of Japan to Tanzania)
Ziko nchi, kama vile Marekani, ambazo tamaduni zao hazina utata juu ya kukosoa, kulalamika, na hata kukemea. Lakini Japan haina jadi hiyo, kwa misingi ya utamaduni wao ambao umejengeka katika dhana kama "saving face." Ukilalamikiwa na Japani, lazima ujitafakari sana, na hapa ndipo mamlaka za Tanzania zimekwama.
Niliwahi kutamka katika ukurasa wangu wa Facebook kuwa mimi kama mtafiti wa tofauti za tamaduni nililichukulia tamko la balozi wa Japani kwa uzito wa pekee kwa mujibu wa utamaduni wao, nikataja kitabu katika maktaba yangu cha utamaduni wa Japani, kilitwacho "Culture and Communication," ambacho kinaonekana pichani.
Baadaye, nilifukua maktaba yangu, nikaona vitabu vingine viwili, vinavyoonekana pia pichani. Katika kuvisoma, nimejithibitishia lile wazo langu kuwa kama hata Japani inalalamika, basi hujuma zilizofanyika katika uchaguzi lazima zilikuwa mbaya kupindukia. Nakaribisha mchango wa yeyote mwenye ujuzi na elimu zaidi, kwani hili ni suala la kitaaluma, na utafiti hauwekewi mipaka.

Wednesday, November 25, 2020

Kitabu Kujadiliwa Chuoni St. Olaf

Tarehe 8 Januari, kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences kitajadiliwa katika semina ya maprofesa wa chuo cha St. Olaf Nitaendesha hiyo semina ili kuleta mitazamo mipya juu ya migogoro ambayo waMarekani wana jadi ya kuijadili kama matokeo ya ubaguzi wa rangi. Suala la tofauti za tamaduni hawaliwazii. Semina yangu italenga kuleta dhana hiyo.

Semina hii ni moja ya semina zinazoendeshwa kwa ufadhili wa Institute for Freedom and Community hapa chuoni. Kwa kawaida, semina hizi zinahusu mada za kitaaluma. Lakini hii semina yangu inahusu mahusiano ya watu ya kila siku, bila kupotelea kwenye mawingu ya nadharia. Profesa moja mstaafu, maarufu katika taaluma ya falsafa, baada ya kukisoma kitabu changu aliniambia kuwa tunahitaji kitabu cha aina hii.

Hii ni fursa ya kukitaambulisha kitabu changu rasmi hapa chuoni, ingawa kuna watu ambao wamekuwa wakikisoma.

Saturday, November 21, 2020

Alex Trebek wa "Jeopardy" Afariki

Alex Trebek, mwendeshaji wa kipindi cha televisheni cha "Jeopardy" amefariki, akiwa na miaka 80.  Kwa hapa Marekani, "Jeopardy" ni kipindi maarufu sana, ila mimi sikuwa najua. Nilikuja kuzinduka tarehe 23 Novemba, 2017.

Kumbe siku hiyo Trebek alikitaja kitabu changu Matengo Folktales katika kipindi chake. Watu mbali mbali walioshuhudia walianza kupeana na taarifa na mimi nikazipata. Pongezi zilifika kwa wingi, na ndipo nami nikafahaamu maana ya kutajwa kwenye kipindi hicho.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...