Raha ya Kununua Vitabu

Tangu nilipokuwa kijana mdogo, nilipenda kununua na kusoma vitabu. Niliwahi hata kununua vitabu ambavyo vilikuwa vigumu mno kwangu kuvielewa. Nakumbuka, kwa mfano, kitabu kimoja cha falsafa, kilichoandikwa kiIngereza, ambacho nilinunua ila nilipata taabu sana kukisoma. Pamoja na kuwa somo la kiIngereza nilikuwa nalipenda na kuliweza kuliko masomo yote, kitabu hiki kilinishinda kwa wakati ule wa ujana wangu. Lakini nilifurahi kuwa nacho katika maktaba yangu ndogo. Nilinunua pia vitabu vya kiSwahili. Kwa mfano, nakumbuka vizuri kitabu cha Shaaban Robert, Maisha Yangu . Vile vile, nakumbuka kitabu cha Yusuf Ulenge , Nguzo ya Maji na Hadithi Nyingine . Wakati ule, sikujua kabisa kuwa Yusuf Ulenge alikuwa mdogo wa Shaaban Robert. Hayo nimekuja kujua mwaka 2008, baada ya kununua na kusoma kitabu kiitwacho Barua za Shaaban Robert 1931-1958 , kilichochapishwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili , Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa mara ya kwanza mwaka 2002. Nimefurahi sana kufahamu kuwa Yusu