Mungu ni Mmoja Tu
Dini ni kati ya masuala ninayopenda kuyaongelea katika blogu hii. Kwa kitambo sasa, nimekuwa nikielezea imani yangu kwamba kuna Mungu mmoja tu. Nimekuwa nikielezea ulazima wa kuziheshimu dini zote. Nilikuwa nikisema hayo yote nikiwa najitambua kuwa ni m-Katoliki. Sijui wa-Katoliki wenzangu walinionaje, na sijui wa-Kristu wenzangu walinionaje. Sijui watu wa dini zingine walinionaje. Ninafurahi kwamba mkuu wa kanisa Katoliki, Papa Francis, ana mwelekeo huo huo. Dalili za mwelekeo wake zilianza kujitokeza tangu mwanzo wa utumishi wake kama Papa. Aliongeza kasi ya kujenga mahusiano baina ya dini mbali mbali, akifuata mkondo ulioanzishwa na mapapa waliotangulia. Leo nimeona taarifa kuwa Papa Francis ameweka msimamo wake kuhusu dini mbali mbali kwa uwazi kuliko siku zilizopita. Amesema kuwa dini zote ni njia mbali mbali za kumwelekeza binadamu kwa Mungu. Nimeona kuwa msimamo huu ni changamoto kubwa ambayo inahitaji kutafakariwa. Kwa kuzingatia mtazamo huu wa Papa Francis, ninaona k