Polisi Wajifunze Nidhamu, Wazingatie Haki
Mara kadhaa, hasa wakati wa kampeni za kisiasa na uchaguzi, tumeshuhudia vitendo vya polisi na vyombo vingine vya dola ambavyo vimechangia kuleta hofu miongoni mwa wananchi na pia kuvuruga amani. Katika uchaguzi wa mwaka huu, vitendo hivi vimejitokeza tena, kama inavyoonekana katika video hii Kwanza namsifu na kumshukuru huyu dada anayeongea katika video hii kwa kutuelezea hayo anayoelezea, kwa uwazi na kwa dhati. Nafikiri ametoa somo la maana sana, na nategemea wahusika watajirekebisha. Kama wahenga walivyosema, kosa si kufanya kosa, bali kurudia kosa. Kwa upande mwingine, ni lazima niseme kuwa, kwa ujumla, kazi ya polisi si rahisi. Katika mazingira kama haya ya kampeni za siasa na uchaguzi, hali inaweza kuwa ngumu pia, kwa sababu ya ushindani mkubwa na pengine uhasama unaoweza kuwepo katika jamii. Kwa hivi, naamini kuwa polisi wanaweza kufanya maamuzi au vitendo kwa lengo la kulinda amani, kumbe ikawa vitendo vyao vikachangia kuharibika kwa amani. Hata hivi, naamini kuwa polisi