TAMKO LA JUMUIA NA TAASISI ZA KIISLAM JIJINI MWANZA
Nimeona tamko hili nikaamua kuliweka katika blogu yangu, kwa vile ninaheshimu uhuru na haki ya watu kujieleza. Mimi ni m-Katoliki, na ingawa sikubaliani na kila kilichomo katika tamko hili, nimeona lina mengi ya kufikirisha, kwa manufaa ya Taifa letu. Hatuwezi kukwepa ukweli kwamba ni Taifa la watu wa imani mbali mbali na mitazamo mbali mbali, na kwa hivi, pamoja na tofauti zetu, lazima tutafute namna ya kuishi pamoja kwa maelewano. Hatua moja ni kusikiliza maoni ya kila mtu, kwa utulivu na kuheshimiana. Ndio maana nachangia kueneza tamko hili. --------------------------------------------------------------------------------------- TAMKO LA JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAMU JIJINI MWANZA KUHUSU HALI YA KISIASA, KAULI ZA MAASKOFU, NA MUSTAKBALI WA NCHI LILILOTOLEWA JUMAPILI TAREHE 23 JANUARI, 2011 KATIKA VIWANJA VYA SHULE YA MSINGI MBUGANI (MUSLIM SCHOOL), JIJINI MWANZA UTANGUZI: Mwaka 2010 ulikuwa mwaka wa Uchaguzi wa viongozi wa ngazi mbali mbali wakiwemo madiwani, wabunge, wawakilishi