Tuesday, November 3, 2009

Kijitabu Kuhusu "Things Fall Apart"

Riwaya ya Chinua Achebe, Things Fall Apart, inafahamika duniani kote. Inatumika sana mashuleni. Mimi kama mwalimu wa fasihi nimefundisha riwaya hii kwa miaka mingi, hadi nikaandika mwongozo kwa wasomaji, wanafunzi, na walimu. Mwongozo huu ni kijitabu ambacho kinapatikana mtandaoni. Bofya hapa.

Lakini, kama watu wasemavyo, tunakwenda na wakati. Tarehe 1 Novemba, 2009 nimekichapisha kijitabu hiki kama "e-book." Yeyote mwenye kifaa kiitwacho "e-reader," au "e-book reader," anaweza kukiingiza katika kifaa hicho, akakisoma. Bofya hapa.

2 comments:

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

prof, nashinddwa kuchapisha vitabu bwana. kila nikijaribu sijaweza ila ntafanikiwa tu, sijajua kama ni lazima uwe kwenye PDF au la

Mbele said...

Hebu ngoja nihangaike na shughuli zinazonikabili kwa sasa, halafu nitakuandikia maelekezo. Nikichelewa baada ya wiki moja hivi, nibonyeze.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...