Taifa la Kesho
Wahenga walisema, mtoto umleavyo ndivyo akuavyo. Picha hii inatueleza mengi kuhusu malezi ya watoto katika jamii yetu. Ni kawaida kwa watoto katika Tanzania kuonekana kwenye baa, na kwenye miziki, hata usiku wa manane. Humo mitaani wanashuhudia mambo ya ajabu mengi, kuanzia ulevi, matusi, na hata watu kuumizwa au kuuawa kwa tuhuma za wizi. Kuwapiga au kuwaua wezi imeshakuwa kivutio kikubwa mitaani, kama vile burudani. Haya ndio malezi ya watoto wa leo. Watakapokuwa watu wazima, itakuwaje? Picha hapo juu niliiona kwenye blogu fulani, ila nimesahau. Nitapenda kutafuta chanzo ili niweke taarifa kikamilifu.