Wednesday, July 22, 2009

Picha kutoka Tamasha la Utalii (KTTF) 2009

Tarehe 5-7 Juni, kulifanyika tamasha la utalii Arusha, Tanzania. Tamasha hili hufanyika kila mwaka mwanzoni mwa mwezi Juni.

Wahusika wa Programu ya Utalii Mto wa Mbu walishiriki tamasha hilo. Leo wameniletea picha za kumbukumbu.






4 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Safi sana nimefurahi kuona kazi inasonga mbele.

Mbele said...

Dada Yasinta, shukrani kwa ujumbe wako. Inaleta faraja kuungana na watu walioko nyumbani na kufanya mambo pamoja. Hao ndugu wa Mto wa Mbu tumeanza mbali. Tulianzia na kufahamiana, kuelewana falsafa na malengo, na sasa tunajisogeza katika utekelezaji, huku tukiendelea kujifunza.

mica172024 said...

Hi Josep

Nafurahi sana nikisia habari ya kazi yako pamoja na matunda yake, Tafadhali tuwasiliane mara kwa mara na kuangalia ni namna gani tunaweza kuwawezesha wenzetu wanaonesha juhudi za kusonga mbele.

Mbele said...

Ndugu mica172024, shukrani kwa ujumbe wako. Napenda watu wa aina yako, ambao wanataka ushirikiano. Uwezo tunao, na penye nia pana njia. Tuwasiliane.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...