Saturday, June 15, 2019

Wenzetu Wanasoma Vitabu

Nilikwenda Mall of America  Juni tarehe 8, nikapitia kwenye duka la Half Price Books mjini Apple Valley, kama ilivyo kawaida yangu.

Nilianzia sehemu ambapo vinawekwa vitabu vya Ernest Hemingway, halafu nikaenda sehemu yenye vitabu vilivyopunguzwa bei zaidi ("clearance."). Halo niliona hali inayoonekana pichani, watu wakiwa wanapekua na kuangalia vitabu, na wengine wakisubiri fursa hiyo.

Hao wenzetu wamelelewa hivyo. Wanaona vitabu ni muhimu maishani mwao. Dunia ya leo na kesho ni ya maarifa na ujuzi. Itawaendea vizuri wanaowekeza katika elimu. Utamaduni wa kusoma vitabu uwe kipaumbele cha wote.


Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...