Changamoto za Kuendesha Blogu
Kuenesha blogu sio kazi rahisi. Kuna changamoto nyingi. Kwa mfano, wakati mwingine unashindwa kujua uandike nini. Huna wazo kichwani. Wakati mwingine unaandika ukijiuliza kama kweli uchapishe hicho unachoandika. Unajua fika kuwa chochote unachochapisha, kinasambaa duniani dakika hiyo hiyo. Kuna pia upande wa wasomaji, yaani hao tunaowaita wadau wa blogu. Binafsi, nawakaribisha wadau wanaotembelea blogu yangu. Unapoandika makala kwenye blogu yako, huwezi kujua watu wataipokea vipi. Kila mtu ni tofauti na mwingine. Kinachomridhisha au kumpendeza huyu kinaweza kumuudhi mwingine. Ufanyeje hapo? Huwezi kumridhisha kila mtu, na kwa upande wangu siandiki kwa lengo la kumridhisha yeyote. Najaribu tu kuelezea kilichomo akilini au moyoni mwangu wakati ninapondika. Kuna pia wadau wanaoandika maoni. Hapo pana changamoto. Kuna watoa maoni ambao wanamshambulia au kumbeza mwendesha blogu. Je, ni sahihi kwa mwendesha blogu kuyafuta maneno yao yasionekane kwenye blogu? Bin