Watu wanaokaa Tanzania wanaweza wasielewe umuhimu wa blogu kuweka picha kama hizi ninazoweka hapa. Lakini wale wanaoishi ughaibuni, wanaguswa, kwani wako mbali. Mimi mwenyewe sikosi kungalia blogu kama ya Mjengwa, kwa jinsi inavyoleta picha kutoka sehemu mbali mbali hasa za Uswanzi za vijijini, pamoja na kule kunakovunjika jembe ukabaki mpini.
Sunday, March 25, 2012
Nimetua Safari Resort Dar es Salaam
Watu wanaokaa Tanzania wanaweza wasielewe umuhimu wa blogu kuweka picha kama hizi ninazoweka hapa. Lakini wale wanaoishi ughaibuni, wanaguswa, kwani wako mbali. Mimi mwenyewe sikosi kungalia blogu kama ya Mjengwa, kwa jinsi inavyoleta picha kutoka sehemu mbali mbali hasa za Uswanzi za vijijini, pamoja na kule kunakovunjika jembe ukabaki mpini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...
7 comments:
Ahsante kwa kutuletea/kutukumbusha Safari Resort,Vipi kuhusu Bahama Mama bado ipo na jina ni lilelile?Uwe na wakati mwema Ndugu.
Picha nzuri na kumbukumbu nzuri sana. Ahsante sana ...Uwe wakati mzuri.. pamoja daima
Asanteni kwa kunitembelea hapa kijiweni pangu. Dada Rachel, nimeanza kufuatilia suala la Bahama Mama. Nilimwuliza dada moja, akasema alisikia iko katika kukarabatiwa. Napangia kwenda kesho au keshokutwa, nikajionee. Kama iko bado inadunda, nitaleta picha.
Ahsante sana Ndugu yangu,Mungu akubariki sana na uwe na wakati mwema.
rachel bahama mama ipo lakini sio kama zamani....
Ahsante Anonymous kwa kunifahamisha.
Sisi tulipofika pale kwenye kituo cha mafuta, tuliona Bahama Mama imezuiwa na ukuta wa mabati. Hatukuwa tena na wazo la kujaribu kutafuta kama kuna sehemu ya kuingilia, tukaamini inakarabatiwa.
Ningekuwa radhi kwenda tena kuangalia haya mabati yanafanya nini pale hata watu tudhani pamefungwa. Hali ilivyo ni kwamba najiandaa kwa safari ya kurejea ughaibuni wikiendi hii.
Post a Comment