
Nimeshatembelea Faribault mara kadhaa, kutoa mihadhara na kushiriki shughuli zinazohusu elimu kwa jamii na hata kusuluhisha migogoro inayotokana na tofauti ya tamaduni, kama inavyoelezwa hapa na hapa.
Kwa hapa Marekani, ni jambo la kawaida kuwaita waandishi kuongelea vitabu vyao. Huwa ni fursa ya kukutana ana kwa ana na mwandishi, kuuliza masuali, na kununua vitabu.
Kitu kimoja kinachowavutia sana wa-Marekani ni kununua kitabu wakati huo na kumpa mwandishi aandike jina lake na pia ujumbe kwenye nakala ya kitabu hicho.
Kuhusu shughuli ya hiyo tarehe 21 Oktoba mjini Faribault, Mama Delane James, mkurugenzi wa maktaba ya Faribault, ameandika mwaliko huu katika ukumbi wa Facebook:
Dear Friends:
I hope you will be able to join us in the Great Hall at 6:30 p.m. as St. Olaf Professor Mbele speaks about his book, Africans and American: Embracing Cultural Differences.
Professor Mbele visited with our library staff last spring and we all agree... he is incredible! We are thrilled to be hosting this event and hope you can make it!
--Delane
2 comments:
Nakutakia kila la kheri natamani ningekuwa huko na kukusikiliza.
Dada Yasinta, shukrani kwa ujumbe wako. Lakini napenda kusema kuwa nangojea kwa hamu kitabu utakachoandika. Jipigepige, maana una uzoefu na ufahamu wa mengi ya ulimwengu huu.
Post a Comment