Najaribu kutafakari picha hii iliyopigwa katika moja ya mikutano ya kampeni za uchaguzi zinazoendelea Tanzania. Ina maana kwamba mwenye uwezo wa kupiga "push-up" nyingi ndio anafaa kuwa kiongozi? Je, ili uukwae ubunge, unatakiwa upige angalau "push-up" ngapi? Udiwani je? Na ili uwe waziri, unahitaji "push-up" ngapi? Na kwa uwaziri, ni sahihi tuwe na "push-up" tu au na kuruka viunzi pia? Na kwa kuzingatia uzito wa cheo cha uwaziri, kwa nini tusiongezee pia uwezo wa kunyanyua matofali angalau manne ya zege? Kwa kweli, tukifanya hivyo, tutapata serikali imara kabisa.
Showing posts with label uchaguzi Tanzania. Show all posts
Showing posts with label uchaguzi Tanzania. Show all posts
Monday, September 28, 2015
Kampeni za CCM Mwaka Huu
Najaribu kutafakari picha hii iliyopigwa katika moja ya mikutano ya kampeni za uchaguzi zinazoendelea Tanzania. Ina maana kwamba mwenye uwezo wa kupiga "push-up" nyingi ndio anafaa kuwa kiongozi? Je, ili uukwae ubunge, unatakiwa upige angalau "push-up" ngapi? Udiwani je? Na ili uwe waziri, unahitaji "push-up" ngapi? Na kwa uwaziri, ni sahihi tuwe na "push-up" tu au na kuruka viunzi pia? Na kwa kuzingatia uzito wa cheo cha uwaziri, kwa nini tusiongezee pia uwezo wa kunyanyua matofali angalau manne ya zege? Kwa kweli, tukifanya hivyo, tutapata serikali imara kabisa.
Thursday, October 28, 2010
Mgombea wa CCM Kufanya Mahojiano
Zikiwa zimebaki siku tatu tu hadi uchaguzi ufanyike nchini Tanzania, tumepata habari kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM atafanya mahojiano na vyombo vya habari. Hii ni tofauti na msimamo wa CCM katika kipindi chote cha kampeni, ambapo wagombea wake walikuwa hawashiriki midahalo.
Wengi wetu tunafahamu kuwa midahalo, mahojiano, na kadhalika, ni mambo muhimu katika jamii inayothamini elimu. Sasa kwa nini CCM haikutambua hilo kabla? Tena CCM ni chama chenye wanachama milioni kadhaa, wakiwemo "wasomi" wengi.
Ni lazima niulize: hao ni wasomi kweli au ni wababaishaji? Ni aibu kuwa hawakuweza kuchangamka kabla na kutambua umuhimu wa midahalo, hadi saa hii ya mwisho, na baada ya Dr. Slaa kuonyesha mfano.
Mimi kama mwalimu, na pia raia ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, nawajibika kuwashutumu CCM kwa kutoonyesha mfano bora, pale walipotamba kuwa mgombea wao hahitaji kushiriki midahalo. Na pamoja na hayo, wagombea wao wote wakawa hawashiriki midahalo. Sijui kama ilikuwa ni fikra zao au ndio nidhamu ya chama. Kama ndio nidhamu ya chama, ni heri nibaki bila chama, kuliko kuwa katika himaya ya udikteta.
Narudia kuushutumu uamuzi wa kutoshiriki midahalo. Na hao wagombea wote nawashutumu kwa kutii amri isiyo na busara kama hiyo. Je, sasa, kwa vile JK ameamua kufanya mahojiano, nao watakimbilia kwenye vyombo vya habari kufanya mahojiano? Akili gani hiyo? Mimi kama mwalimu, lazima niulize: tunawafundisha nini watoto wetu, ambao ni taifa la kesho?
Baada ya kusema hayo, mimi kama raia mwema, ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, nina masuali kwa mgombea wa CCM. Kwa vile hakuna muda wa kuuliza yote, nitauliza matatu tu.
La kwanza ni kwa nini wale ambao Dr. Slaa amewataja katika orodha yake ya mafisadi hawajampeleka mahakamani hadi leo?
La pili ni je, kwa nini CCM inadai kuwa amani Tanzania inatokana na uongozi wa CCM, wakati CCM inashiriki kikamilifu katika kuhujumu amani, hasa nyakati za kampeni na uchaguzi? Mifano ni mingi, kuanzia Visiwani hadi Bara, na hata ripoti za kimataifa zinathibitisha hilo. Kwa mfano, soma hapa na pia angalia video hizi hapa.
Ukweli ni kitu muhimu sana. Je, CCM haitambui kuwa wanaotunza amani Tanzania kikweli kweli ni sisi mamilioni ya raia ambao si wanachama wa chama chochote cha siasa? Hatuna rekodi yoyote ya kuvuruga amani kama wenzetu wenye vyama wanavyofanya. Kwa nini CCM inafunika ukweli huo?
Suali la tatu ni je, CCM ina maelezo gani kuhusu shutuma alizotoa Mwalimu Nyerere dhidi ya CCM katika kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania? Kuzifahamu kwa ufupi shutuma hizi, soma hapa.
Wengi wetu tunafahamu kuwa midahalo, mahojiano, na kadhalika, ni mambo muhimu katika jamii inayothamini elimu. Sasa kwa nini CCM haikutambua hilo kabla? Tena CCM ni chama chenye wanachama milioni kadhaa, wakiwemo "wasomi" wengi.
Ni lazima niulize: hao ni wasomi kweli au ni wababaishaji? Ni aibu kuwa hawakuweza kuchangamka kabla na kutambua umuhimu wa midahalo, hadi saa hii ya mwisho, na baada ya Dr. Slaa kuonyesha mfano.
Mimi kama mwalimu, na pia raia ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, nawajibika kuwashutumu CCM kwa kutoonyesha mfano bora, pale walipotamba kuwa mgombea wao hahitaji kushiriki midahalo. Na pamoja na hayo, wagombea wao wote wakawa hawashiriki midahalo. Sijui kama ilikuwa ni fikra zao au ndio nidhamu ya chama. Kama ndio nidhamu ya chama, ni heri nibaki bila chama, kuliko kuwa katika himaya ya udikteta.
Narudia kuushutumu uamuzi wa kutoshiriki midahalo. Na hao wagombea wote nawashutumu kwa kutii amri isiyo na busara kama hiyo. Je, sasa, kwa vile JK ameamua kufanya mahojiano, nao watakimbilia kwenye vyombo vya habari kufanya mahojiano? Akili gani hiyo? Mimi kama mwalimu, lazima niulize: tunawafundisha nini watoto wetu, ambao ni taifa la kesho?
Baada ya kusema hayo, mimi kama raia mwema, ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, nina masuali kwa mgombea wa CCM. Kwa vile hakuna muda wa kuuliza yote, nitauliza matatu tu.
La kwanza ni kwa nini wale ambao Dr. Slaa amewataja katika orodha yake ya mafisadi hawajampeleka mahakamani hadi leo?
La pili ni je, kwa nini CCM inadai kuwa amani Tanzania inatokana na uongozi wa CCM, wakati CCM inashiriki kikamilifu katika kuhujumu amani, hasa nyakati za kampeni na uchaguzi? Mifano ni mingi, kuanzia Visiwani hadi Bara, na hata ripoti za kimataifa zinathibitisha hilo. Kwa mfano, soma hapa na pia angalia video hizi hapa.
Ukweli ni kitu muhimu sana. Je, CCM haitambui kuwa wanaotunza amani Tanzania kikweli kweli ni sisi mamilioni ya raia ambao si wanachama wa chama chochote cha siasa? Hatuna rekodi yoyote ya kuvuruga amani kama wenzetu wenye vyama wanavyofanya. Kwa nini CCM inafunika ukweli huo?
Suali la tatu ni je, CCM ina maelezo gani kuhusu shutuma alizotoa Mwalimu Nyerere dhidi ya CCM katika kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania? Kuzifahamu kwa ufupi shutuma hizi, soma hapa.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...
-
Ukizunguka mitaani Dar es Salaam, utakuta matangazo mengi ya waganga wa kienyeji. Waganga hao wanatoka sehemu mbali mbali, kama vile Sumbaw...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Jina la Shaaban Robert ni maarufu miongoni mwa wa-Tanzania na wengine wa nchi zingine wanaokijua ki-Swahili. Lakini, tujiulize ni wa-Tanza...