Wednesday, December 16, 2015

Nimeitafsiri Sala ya Papa Francis

Nilielezea katika blogu hii nia yangu ya kuitafsiri sala ya Papa Francis ambayo ni sehemu ya waraka wake wa kitume, "Laudato Si." Papo hapo, ninafahamu vizuri kuwa kutafsiri ni suala tata. Katika ujumbe wangu, niliandika kuwa

"napenda kusema kwamba sala hii ilivyo katika ki-Ingereza ikiwa imesheheni uchaji, busara, na maudhui, imeundwa kwa lugha iliyotukuka. Ninajiuliza iwapo tunaweza kuitafsiri kwa ki-Swahili, tukahifadhi utukufu wake kwa msingi wa uhalisia wa ki-Swahili. Ninajiuliza hivyo pamoja na kufahamu jinsi suala la tafsiri lilivyo gumu na tata. Ninatarajia kujaribu kuitafsiri sala hii siku zijazo."

Hata hivi, nimejaribu kutafsiri sala ya Papa Francis, ili kuwapa angalau fununu wale ambao hawajui ki-Ingereza. Ni bora kufanya hivyo, kuliko kuacha kabisa. Ye yote anayekijua ki-Ingereza vizuri, na pia anakijua ki-Swahili vizuri, ataona kuwa nimejipa mtihani mgumu. Ninamhimiza naye ajaribu kutafsiri.

A prayer for our earth

All-powerful God, you are present in the whole universe
and in the smallest of your creatures.
You embrace with your tenderness all that exists.
Pour out upon us the power of your love,
that we may protect life and beauty.
Fill us with peace, that we may live
as brothers and sisters, harming no one.
O God of the poor,
help us to rescue the abandoned and forgotten of this earth,
so precious in your eyes.
Bring healing to our lives,
that we may protect the world and not prey on it,
that we may sow beauty, not pollution and destruction.
Touch the hearts
of those who look only for gain
at the expense of the poor and the earth.
Teach us to discover the worth of each thing,
to be filled with awe and contemplation,
to recognize that we are profoundly united
with every creature
as we journey towards your infinite light.
We thank you for being with us each day.
Encourage us, we pray, in our struggle
for justice, love and peace.

Sala Kuiombea Dunia Yetu

Mungu mweza yote, upo kila mahali

na hata katika viumbe vyako vidogo kabisa.
Unakumbatia kwa upole wako kila kilichopo.
Tufurikie nguvu ya upendo wako
ili tuuhifadhi uhai na uzuri.
Tujaze amani, ili tuishi
kama kaka na dada, bila kumdhuru yeyote.
Ee Mungu wa maskini,
tusaidie kuwanusuru waliotelekezwa na kusahauliwa katika dunia hii,

ambao wana thamani isiyo kifani machoni mwako.
Tuletee uponyaji maishani mwetu,
ili tuihifadhi dunia badala ya kuwania kuipora,
ili tustawishe uzuri, si uchafuzi na uharibifu.
Gusa mioyo
ya wale wanaowania maslahi yao tu
yanayowagharimu maskini na dunia.
Tufundishe kuibaini thamani ya kila kitu,
kujawa na uchaji na tafakari,
kutambua
 kuwa tumefungamana
na kila kiumbe
tunavyoelekea kwenye nuru yako isiyo na mwisho.
Tunakushukuru kwa kuwa nasi kila siku.

Tuhimize, tunakuomba, katika juhudi zetu
za kutafuta haki, upendo na amani.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...