Friday, August 9, 2013

Afrifest 2013, Minnesota

Kesho, Agosti 10, ndio ile siku ya tamasha la Afrifest hapa Minnesota. Ni tamasha linalofanyika mara moja kwa mwaka, kwa lengo la kuwakutanisha watu wenye asili ya Afrika na wengine pia. Afrifest ni fursa ya kufahamiana, kuelimishana, na kuburudika na maonesho mbali mbali ya michezo na tamaduni.

Kwa taarifa zaidi kuhusu tamasha la kesho, angalia tangazo nililobandika hapa. Pia soma nilivyoandika katika blogu yangu ya ki-Ingereza.

Kama una watoto, na unakaa maeneo haya ya Twin Cities, jiulize watoto hao wana fursa zipi za kupanua mawazo ili wawe raia wa dunia ya utandawazi wa leo. Unawaandaa vipi waweza kuwa na uzoefu wa kufanya kazi na kushirikiana na watu wa mataifa na tamaduni mbali mbali.

Ni wazi kuna vitu vikubwa ambavyo mzazi unaweza kufanya kwa lengo hilo. Lakini vile vile, kuna vitu kama haya matamasha ambayo yanachangia. Mimi kama mtafiti, mwalimu na mwandishi nahudhuria Afrifest kila mwaka. Napata fursa ya kufahamiana na watu, kukutana na wale ambao tunafahamiana, kuongelea shughuli zangu, na kuonesha vitabu na machapisho yangu mengine.

Kati ya vivutio vikubwa vya kesho ni kuwa Seneta Al Franken wa Minnesota atatembelea Afrifest yapata saa 10:30 alasiri hadi saa 11:00. Hiyo ni fursa ya nadra ya kuonana na mtu wa hadhi kama yake katika serikali ya Marekani.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...