Sunday, August 4, 2013

Mapendekezo ya Mwigulu Nchemba Kuhusu Ajira kwa Vijana

Jana, kwenye ukurasa wake wa Facebook, Mwigulu Nchemba ametoa mapendekezo kuhusu ajira, ambayo anasema atayawasilisha Bungeni kama hoja binafsi:

Habari vijana wenzangu, Nategemea kupeleka HOJA BINAFSI BUNGE LA 26 AUGUST 2013 KUHUSU AJIRA KWA VIJANA.

HINTS,
1) Kuitaka Serikali iitishe sensa ya wahitimu wote wa fani zote na ifanye uchambuzi wa ikama ya utumishi katika wizara, idara, mikoa, halmashauri- serikali za mitaa, na mashirika yake ya Umma. Lengo ni kujua idadi ya wahitimu wasio na kazi na nafasi zilizowazi. Utafiti wangu ni kwamba KWA UPANDE WA SERIKALI;

(A) KILA OFISI ya serikali INASHINDWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE ipasavyo KWA AJILI YA UPUNGUFU WA WATUMISHI, HAKUNA OFISI IMETIMIA WATUMISHI
(B) KUNA WATU WENGI SANA WANAKAIMU NAFASI MPK WENGENE WANAKAIMU NAFASI ZILIZOKUWA ZINAKAIMIWA yaani KAIMU KAIMU AFISA UTUMISHI NK NA NAFASI YAKE HIVYO HIZI NI tatu nafasi kwa mtu mmoja
(C) KUNA WATU wanapewa ajira za mikataba na WANAONGEZEWA MIKATABA KWA KIGEZO KUWA HAKUNA MTU ANAYEWEZA KUZIBA NAFASI HIYO au hakuna mwenye uzoefu.

KWA UPANDE WA PILI SASA WA WAHITIMU;

(1) KILA MTAA KUNA KIJANA AU VIJANA WAHITIMU WANA MIAKA 2 HADI 5 HAWANA KAZI WANAZUNGUKA NA BAHASHA MPAKA SOLI ZA VIATU ZINAKWENDA UPANDE
(2) KILA MTAA VIJANA WAPO WAKIOMBA KAZI WANAAMBIWA HAWANA UZOEFU wa 2 or 3 yrs, Au anayetakiwa awe na 4yrs experience hata katika ngazi za ofisa wa ngazi za kuanzia ilihali hakuna chuo kinafundisha uzoefu
(3) Vijana wapo na diploma hawajulikani walipo kwa Serikali na wamekaa miaka 2 hadi 5 na diploma zao wanasubiri kazi. kipindi ambacho angewezeshwa kwenda shule angeshavuka diploma na degree angekuwa hata na master.

Kufuatia hali hii
(i) vijana wanaitwa bomu ili hali VIJANA NI NGUVU KAZI YA TAIFA
(ii) Vijana wana stress, wamekata tamaa hawaoni future na wengine wanahasira sana
(iii) Vijana wahitimu wanatunzwa na wazee ambao hawakwenda shule hivyo kuwa mzigo kwa wazazi.

Lengo ni kuitaka serikali ikishajua idadi ya wahitimu na ikama yake cos ofisi ziko wazi mlioko ofisini mkisema ukweli msiogope mabosi wenu mtakiri hili

(1) Serikali ifanye re allocation ya vijana kwenye nafasi za kazi kufuatana na ujuzi wao,
(2) Serikali ianze kufanya attachment kwa vijana wapate uzoefu maofisini na hata kuwalipa half a saraly of a full employed officer ili kuondokana na tatizo la kukosa uzoefu kwa kijana aombapo kazi.
(3) Vijana wawe tayari kujitolea kulipwa hata half a saraly ili wapate uzoefu
(4) Uwezo wa kazi na marks za kwenye vyeti ni vitu viwili tofauti, serikali ikiwa attach ofisini vijana itajua uwezo wao itaacha kuongezea wastaafu mikataba kwa vigezo kuwa hakuna mwenye uwezo wa kuziba nafasi hiyo
(5) Serikali ibane matumizi yake ili itenge fedha ya kuendeleza wahitimu. Mtu mwenye diploma kusubiri kazi miaka 5 ni kipindi angeweza kuwa na degree na masters yake.
Baadhi sehemu za kukata matumizi ya serikali bila kuathiri kazi za serikali ni kwenye magari na mafuta ya magari. Unakuta bosi anakaa bunju halafu dreva gongolamboto halafu ofisi posta, au bosi kiluvya dreva mbagala ofisi posta kila siku trip hizo, pia training nje ya nchi kwa mtu mwenye 59yrs nakutumia milions and milions zisitishwe ili tuandae generetion ya kupokea majukumu.
Pia serikali ikishajua waliopo pia iandae projection ya tunakoelekea in three to five yrs hali itakuwaje na serikali inampango gani. Cos maisha bora yanaletwa na KAZI.
SERIKALI IKISHAJUA IWEKE BAJETI AMA YA GUARANTEE AU YA KUFUFUA VIWANDA VYOTE VILIVYO LABOUR INTENSIVE ili kuchukua vijana wahitimu na wa mtaani. SENSA HII SIO GHARAMA NI KUWATANGAZIA TU WAHITIMU WAKAJIANDIKISHE KTK OFC ILIOKARIBU AU KUPELEKA CV kwa DC the cv zinachambuliwa.

This is a rough idear. You can add or improve.

VIjanaaaaaaaa, itikieni NGUVU KAZI YA TAIFA

********************************************************************
Nami nimemjibu katika ukurasa huo huo wa Facebook kama ifuatavyo
:


Kwanza kabisa, andika ki-Swahili ipasavyo, sio kuchanganya na maneno ya ki-Ingereza, kama ufanyavyo. Tunapaswa kuonyesha kuwa tunaiheshimu lugha yetu. Kiswahili kinajitosheleza, sawa na lugha zingine. Lugha ni kioo cha nafsi na upekee wa jamii au taifa. Kuiheshimu lugha ni dalili ya kujiheshimu.

Hasa kwa mtu anayehesabiwa kuwa ni kiongozi, sherti kuonyesha mfano katika hili. Kama kiongozi unashindwa kuonyesha heshima kwa lugha yetu, unashindwa kuonyesha heshima wa utambulisho huu wa Taifa letu, ni kiongozi gani, na unawafundisha nini watoto wetu?

Ujumbe wako kuhusu ajira unapwaya sana. Hujaweka suala hili katika mkabala wowote, wala hujalifanyia utangulizi unaoonyesha kuwa unaelewa historia na upana wa suala hili. Hata dhana yenyewe ya ajira unayotumia ni finyu. Papo hapo unadai kuwa umefanya utafiti. Ni ajabu.

Hujazingatia tulikotoka, kwa Mwalimu Nyerere, ambaye aliongelea masuala haya ya ajira. Aliongelea masuala ya elimu kwa vijana, akisisitiza kuwa tuwape elimu ya kujitegemea. Inaonekana hujasoma lolote kuhusu mawazo ya Mwalimu Nyerere juu ya suala hili la elimu ya kujitegemea.

Ungefanya utafiti kuhusu kinchoendelea duniani, angalau ungegundua kuwa katika dunia ya leo, watu huongelea umuhimu wa kutoa elimu kwa vijana kwa lengo la kuwawezesha kujiajiri, kujitengenezea ajira.

Hilo hujataja, na haionekani unalifahamu. Wewe unaongelea ajira serikalini. Dhana hiyo, ingawa ilikuwa na mantiki kubwa miaka ya zamani, inapitwa na wakati. Na wewe kama kiongozi, ulipaswa utambue hilo, ili uweze kutoa ushauri mwafaka kwa hao vijana.

Unajiita kijana, lakini mawazo yako ni yale yaliyokuwa yanakubalika karne iliyopita, sio mawazo ya karne ya 21. Katika karne ya 21 kuwajengea vijana dhana kuwa waelekeze nguvu katika kutafuta ajira serikalini ni upotoshaji. Hii dhana kwamba Tanzania inahitaji viongozi vijana ni upuuzi, kama vijana wenyewe ni akina Mwigulu Nchemba. Hawafai kuongoza, kwa sababu hawajui dunia ikoje na inakwenda wapi.

Ingekuwa Mwigulu Nchemba unajua dunia ya leo ikoje na inakwenda wapi, kuhusu hili suala la ajira, ungefahamu kuwa sekta inayokuwa kwa kasi kuliko zote hapa duniani ni utalii. Hujataja jambo hilo, ambalo liko wazi miongoni mwa wote wanaofuatilia maendeleo ya uchumi na ajira katika karne hii.

Sekta ya utalii ndio inayokua kwa kasi kuliko zote, na ndio inayoleta matumaini ya kutoa ajira nyingi kuliko hiyo serikali ambayo ndio msingi wa mapendekezo yako.

Kama mtu unataka kutoa mchango katika suala la ajira kwa vijana, ni muhimu sana kuwafungua macho kuhusu sekta hii ya utalii, na jinsi ya wao kujiandaana kujipanga kunufaika na sekta hii.

Sisemi kuwa suala la ajira serikalini lisahauliwe. Lakini ninachosema ni kuwa tuwe na upeo mpana, upeo wa kuelewa hali halisi ya dunia ya leo. Tuwe pia watu ambao tumesoma yale aliyosema Mwalimu Nyerere kuhusu elimu ya kujitegemea.

Mwigulu ukiwa ni katibu mwenezi, nilitegemea unaeneza mawazo thabiti ya kuliendeleza Taifa. Lakini naona unaeneza mawazo rejareja, baadhi yakiwa yamepitwa na wakati. Mtu kama wewe hufai kuwa kiongozi. Wala usije ukadhani mimi ni CHADEMA. Mimi ni raia ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, ila nawashuhudia CCM mnavyojikanyaga.

Ninapenda kusema neno moja zaidi kuhusu Nyerere. CCM mmemsaliti Mwalimu Nyerere. Yeyote anayesoma "Azimio la Arusha" na maandishi mengine ataliona hilo. CCM ni chama kinachohujumu mapinduzi aliyoyawazia Mwalimu Nyerere.

Ungemsoma Mwalimu Nyerere, ungefahamu kuwa alikuwa anakazana sana kuleta mapinduzi vijinini, ili kuwe na fursa za kiuchumi na ajira, na hivi kupunguza ndoto ya vijana kuhamia mijini. Wewe andiko lako lote kuhusu ajira unawaelekeza vijana waende katika ajira za serikali. Ni kuwavutia waende mijini. Hujasema lolote kuhusu kuboresha maisha ya vijijini, uchumi wa vijijini, na ajira huko huko vijijini.

Kwa kumalizia, ningependa kujua iwapo Mwigulu Nchemba unasoma vitabu vyovyote. Ningependa kujua kama una vitabu nyumbani kwako. Ningependa kujua iwapo tangu mwaka huu uanze hadi leo, umesoma vitabu vingapi.

1 comment:

Anonymous said...

Prof, umesema ukweli japo anaweza kuna na nia na wazo zuri. Ni afadhali ameamua kuiainisha mapema hii hoja ili akiweza aiboreshe. Hoja hii inaonesha uanika uwezo mdogo wa uwelewa Mwingulu. Sasa tunapata majibu ya michango yake bungeni.
Hili ni janga.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...