Friday, August 16, 2013

Nangojea Kukaguliwa "Eapoti"

Wadau, wiki ijayo ninasafiri kwenda Finland, kwenye mkutano, nikitokea uwanja wa ndege wa Minneapolis. Sasa kuna haka kasuala ka waBongo kukaguliwa sana kwenye hivyo viwanja vya ndege. Nasubiri zamu yangu.

Hii mijitu iliyotufikisha hapa imetuhujumu sana waBongo. Nasikia mingine ni mijitu mikubwa serikalini, na mingine eti ni mifanyabiashara. Biashara gani hii kama si uroho wa fisi, ujambazi, na uuaji?

Hii mijitu imechangia kuathirika kwa afya na maisha ya wengi nchini, na kinachoudhi ni kuwa inaachwa iendelee kutanua na kufanya hujuma hizo. Haya ni baadhi ya matunda ya kuwa na CCM madarakani. Nchi hii iko mikononi mwa CCM. Nawapongeza wana-CCM na vikofia vyao, na magwanda yao ya kijani, kwa kutufikisha hapa tulipo.

Miaka yote iliyopita, nilikuwa najivunia kuwa m-Tanzania, kutokana na kazi kubwa aliyofanya Mwalimu Nyerere. Ilikuwa ni heshima kuwaambia watu popote duniani kuwa mimi ni m-Tanzania. Miaka hii ya leo najisikia aibu kuwa m-Tanzania.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...