
Ingawa mchoraji hajataja mambo ya uchaguzi wa madiwani uliofanyika siku chache zilizopita, katuni inayapeleka mawazo yetu kwenye uchaguzi huo, ambao matokeo yake yamekuwa CHADEMA kushinda kata zote nne zilizokuwa zinashindaniwa.
Matokeo hayo hayakunishangaza. Kwa miaka kadhaa, katika pitapita zangu Arusha, nikiongea na madereva wa teksi, mafundi viatu, na wauza mitumba, nimejionea nguvu za CHADEMA katika mji ule. Nilithubutu hata kuandika makala kuhusu nguvu ya CHADEMA mjini Arusha. Makala hiyo ni hii hapa. Niliandika hayo, na leo ninaandika tena, ingawa mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa.
No comments:
Post a Comment