Thursday, July 12, 2012

Arusha ni ya CHADEMA

Juzi usiku hapa Arusha, nilipanda teksi kuelekea hotelini nilikofikia. Humo njiani nilimwuliza dreva wa teksi kuhusu hali ya kisiasa Arusha baada ya mbunge Godbless Lema wa CHADEMA kuachishwa ubunge.

Alinijibu bila kusita kuwa mbunge wa Arusha ni Godbless Lema, pamoja na kuwa halipwi mshahara. Akaongezea kuwa hata ukifanyika uchaguzi, halafu liwekwe jiwe kugombea, likiwa limeandikwa CHADEMA, jiwe hilo litapigiwa kura na kushinda.

Kwangu hizo ni kauli zenye uzito mkubwa. Kwenye masuala ya jamii, nauheshimu sana uchambuzi wa madereva wa teksi. Niliwahi kusema hivyo katika makala hii hapa.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...