Sunday, July 15, 2012

Nimetoka Arusha Salama

Jana nimetoka Arusha, nikasafiri salama hadi Dar es Salaam. Nilikuwa na wasi wasi kiasi kikubwa nilipokuwa kwenye baadhi ya mitaa ya Arusha, kutokana na namna watu wanavyoendesha magari, piki piki, baiskeli, na kadhalika. Kwenye mitaa hiyo, uendeshaji ni wa kutisha, nami nilikuwa nikitembea mitaani kwa woga, roho mkononi.

Nashukuru nimesalimika hadi kuja tena Dar es Salaam, ambapo napo katika sehemu mbali mbali, uendeshaji ni roho mkononi. Lakini naamini Arusha ni zaidi.

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Na ashukuriwe Muumba kwa kukuweka salama.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...