Thursday, July 19, 2012

Nimefika Songea Tena, Alhamdullilah

Jana jioni nimefika Songea tena. Alhamdullilah. Nimeshinda hapa leo. Nimekutana na ndugu na jamaa, na pia Mheshimiwa Sikapundwa, mmiliki wa blogu ya Tujifunze Kusini. Soma taarifa yake hapa.

Asubuhi sana, kabla hatujaamka, nilisikia jogoo akiwika, na wakati huo huo nilimsikia muadhin akitukumbusha wajibu wetu kwa Muumba. Nilimsikia akisema Allah u akbar. Ni jambo jema sana kwetu waumini, iwe ni wa-Kristo au wa-Islam, kukumbuka au kukumbushwa dhana hiyo ya Allah u akbar, kwamba Mungu ndiye mwenye mamlaka juu ya kila kitu, ndiye mwenye uwezo kuliko mwingine yeyote.

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Heri sana kwa kweli kukutana na ndugu na jamaaa. maana sisi wanablogger tumekuwa ndugu kabisa. Wasalie wote Songea:-)

Anonymous said...

The knowledge of God is the wisdom of being, when we look at life from that perspective we may not take the things we think we need so bad so serious , we will not fear things we do not understand as much and most of all we will not hold a hater attitude (capricious jealousy)

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...