Tanzania ni nchi kubwa, yenye mengi ya kuvutia. Mwaka 2008, kwa mfano, nilishuhudia mnada katika mji wa Karatu. Watu walijaa hapo kwenye viwanja vya mnada. Walikuwepo wauzaji na wateja wa bidhaa na huduma mbali mbali. Wengine, kama mimi, tulienda kuangalia. Kulikuwa na mengi ya kuyaona na hata kustaajabia.
Siku ya mnada ni siku muhimu katika maisha ya watu wa sehemu hizo. Nami nikiwa maeneo hayo, sitakosa kuhudhuria.
No comments:
Post a Comment