Tuesday, May 22, 2012

Mnadani Karatu


Tanzania ni nchi kubwa, yenye mengi ya kuvutia. Mwaka 2008, kwa mfano, nilishuhudia mnada katika mji wa Karatu. Watu walijaa hapo kwenye viwanja vya mnada. Walikuwepo wauzaji na wateja wa bidhaa na huduma mbali mbali. Wengine, kama mimi, tulienda kuangalia. Kulikuwa na mengi ya kuyaona na hata kustaajabia.
Mnada hufanyika Karatu kila mwezi, tarehe 7. Katika pitapita zangu katika sehemu kama Mbulu, Karatu na Arusha, nimeona kuwa utamaduni huu wa minada umejengeka sana.










Siku ya mnada ni siku muhimu katika maisha ya watu wa sehemu hizo. Nami nikiwa maeneo hayo, sitakosa kuhudhuria.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...