Ninawawazia watu ninaowaona mitaani, kila mtu akiwa na harakati zake, mategemeo yake, na bila shaka wasi wasi na shida pia. Laiti ingewezekana kuongea na kila mtu na kuzipata habari zake.
Hapa ni Ubungo. Nilipiga picha hii nikiwa ndani ya basi kutokea mikoani. Nilivutiwa na huyu kijana mwenye mkokoteni, akiwa katika kujitafutia riziki. Barabara inavyopinda kushoto inaelekea Chuo Kikuu na Mwenge.
Hapa ni mjini Moshi.
Hapa ni kituo cha mabasi cha Msamvu, Morogoro.
Hapa ni Lyulilo, karibu na Matema Beach, Ziwa Nyasa. Ni siku ya soko, kama nilivyoelezea hapa.

No comments:
Post a Comment