Saturday, May 19, 2012

Mteja Anaporudi Tena

Niliwahi kuandika habari ya hao akina mama wanaoonekana nami katika hii picha, jinsi walivyonitembelea ofisini. Huyu aliyesimama kulia kanipigia simu wiki hii akiulizia upatikanaji wa nakala za kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences". Nakala aliyokuwa nayo imeazimwa na rafiki yake. Anataka nakala nyingine kwa ajili yake na kwa marafiki zake wengine. Mmoja wao anaenda Ghana, aende akifahamu atakayokumbana nayo kule, niliyoelezea kitabuni.

Basi, kwa kuzingatia yale ninayojifunza na kuwahubiria wengine kuhusu huduma kwa mteja, nimelitekeleza ombi hilo haraka na kumpelekea vitabu. Mteja anapokuja tena, kwa hiari yake mwenyewe, ni dalili nzuri. Inamaanisha karidhika au kafurahia huduma. Nawashangaa wanaoamini kuwa wateja huvutwa kwa mitishamba.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...