Tuesday, February 19, 2013

Shule Ngorongoro

Nilipiga picha ya shule hii, tarehe 10 Januari mwaka huu, katika kijiji kimojawapo cha wa-Maasai sehemu ya Ngorongoro.

Yawezekana kuna wa-Tanzania ambao hawajui kuwa wa-Maasai wanajitahidi kuwapa watoto wao elimu ya shuleni. Hayo nimeyaona katika pita pita zangu sehemu mbali mbali katika nchi ya wa-Maasai.

Yawezekana pia wako ambao watasikitika kuona kuwa shule hii ni ya miti na nyasi, badala ya matofali na bati au vigae. Hilo ni suala la kujadiliwa, kwani ni tata.

Nami niliwahi kusema machache kuhusu suala hili. Niliandika makala kuhusu darasa chini ya mti. Soma hapa.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...