
Tulifika Tanzania tarehe 3 Januari, tukapitia maeneo kadhaa aliyopitia mwandishi huyu hapa nchini petu, tukisoma maandishi yake kuhusu safari zake na matukio mbali mbali sehemu hizo. Maandishi hayo ni riwaya, hadithi fupi, insha, na barua.
Ingawa kazi hii ni nzito, yenye vipengele vingi, nina uzoefu nayo. Nilishaendesha kozi ya aina hii siku zilizopita, kwa wanafunzi wa Chuo cha Colorado, kama nilivyoelezea hapa
Hapo pichani wanaonekana wanafunzi niliowaleta mwaka huu. Ilikuwa ni jioni ya tarehe 28 January, wakati nilipowafikisha uwanja wa ndege wa Kilimanjaro, tayari kwa safari ya Marekani. Insha Allah nitaweka picha na maelezo mbali mbali katika blogu hii.
No comments:
Post a Comment