Monday, September 10, 2018

Mdau Wangu Mpya

Juzi, tarehe 8, nilikwenda Coon Rapids, Minnesota, kuhudhuria uzinduzi wa jarida liitwalo L Magazine. Jarida hilo linalohusu zaidi masuala ya uandishi, uchapishaji, na uuzaji wa vitabu, limeanzishwa na Bi Bukola Oriola mwenye asili ya Nigeria anayeishi hapa Minnesota.

Kati ya watu waliohudhuria ni Dr. Artika Tyner, rafiki wa karibu wa Bi Oriola. Dr. Tyner ni "Vice President for Diversity and Inclusion" wa Chuo Kikuu cha St. Thomas. Anaonekana pichani akiwa ameshika tuzo alizopewa hiyo juzi kwa mchango wake kwa jamii.

Alipotambulishwa kwangu kwenye meza nilipoweka vitabu vyangu, tuliongea kiasi kuhusu shughuli zake na zangu. Alinunua vitabu vyangu, zikiwemo nakala 9 za Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Vile vile alielezea hamu yake ya kuendelea kuwasiliana nami ili tutafakari namna ya kushirikiana katika programu zinazohusu Afrika na watu wenye asili ya Afrika yaani wanadiaspora.

Nilitambua kuwa Dr. Tyner ni mmoja wa waMarekani Weusi ambao wana mapenzi ya dhati na Afrika. Hata mavazi yake yanaashiria hivyo. Ametembelea Afrika na anahamasisha programu za kupeleka watu Afrika. Dr. Tyner ni mtu maarufu, na kwa upande wangu kigezo kimoja ni kwamba ameshatoa mhadhara wa TED kuhusu elimu na mabadiliko ya jamii.


Ninafurahi kumpata mdau huyu mpya. Ninategemea kuendelea kubadilishana naye mawazo na uzoefu na kufanya shughuli mbali mbali za kuelimisha.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...