
Mara kwa mara wananialika kuelezea utamaduni wa Afrika, hasa unavyojitokeza katika fasihi simulizi. Nami hupenda kufanya hivyo. Ninauenzi mchango wa Afrika duniani. Afrika ni chimbuko la binadamu. Ni chimbuko la tekinolojia, sayansi, lugha, fasihi, falsafa, na kadhalika.
Hiyo jana nilelezea hayo, nikaleta methali kadhaa kuthibitisha uzito wa falsafa ya wahenga wetu kuhusu masuala ya maisha na maadili. Tulitafakari methali hizo, na mwishoni nilisimulia hadithi iitwayo "The Donkey Who Sinned," iliyomo katika kitabu cha Harold C. Courlander kiitwacho A Treasury of African Folklore. Nayo tuliitafakari, kwa jinsi inavyoonyesha athari za ubabe kwa wale wasio na nguvu. Katika hadithi hiyo, wenye mabavu wanaogopwa hata pale wanapokosea, na asiye na nguvu anadhulumiwa.
No comments:
Post a Comment