Siku kadhaa zilizopita niliandika kuhusu msomaji wa kitabu changu cha Africans and Americans ambaye alisema kinafaa kuliko kile cha Lonely Planet. Bofya hapa. Nilitamka kiutani kuwa Lonely Planet wakae chonjo, maana wamepata mshindani.
Lakini baadaye, nililazimika kuandika tena kuhusu Lonely Planet, baada ya wao kuandika taarifa iliyoudhalilisha mji wetu wa Arusha. Bofya hapa. Hapo uzalendo ulinisukuma kusema kuwa hao sasa wanatuchokoza, na lazima tujizatiti kujibu mapigo.
Dada Subi, ambaye ni mfuatiliaji makini wa maandishi ya wanablogu wa Bongo na pia mshauri wetu tunayempenda na kumheshimu sana, kanibonyeza leo asubuhi kuwa kuna jambo limetokea Lonely Planet, yaani mteja anayepangia kwenda Tanzania anaulizia kitabu au vitabu vya kusoma, ambavyo si vya aina ya Lonely Planet.
Basi, hapo nimeona lazima niingie mzigoni na kuwachangamkia hao Lonely Planet. Sio kuwalazia damu; ni kuwavalia njuga tu. Nimefanya hivyo tayari, kwa kumpa yule mteja taarifa anazohitaji. Bofya hapa. Heshima na shukrani kwa Dada Subi, kama kawaida, na blogu yake maarufu hii hapa.
Showing posts with label Lonely Planet. Show all posts
Showing posts with label Lonely Planet. Show all posts
Saturday, April 10, 2010
Saturday, March 20, 2010
"Lonely Planet" Waidhalilisha Arusha
Leo nimeona taarifa mtandaoni kuwa Lonely Planet hivi karibuni ilitoa taarifa ikiutaja mji wa Arusha katika orodha ya miji isiyofaa duniani. Arusha imeshika namba nane. Bofya hapa. Sikujua kuwa kuna taarifa ya namna hii, hadi leo, nilipoiona katika Jamii Forums. Bofya hapa.
Inaeleweka kwa nini wahusika wa mji wa Arusha na labda wa-Tanzania wengi wanaishutumu taarifa hii ya Lonely Planet. Mji wa Arusha unajulikana kwa utalii, na katika ushindani uliopo duniani, wahusika wote wanajitahidi kuwa na jina zuri, ili wafanikiwe kibiashara.
Pamoja na yote hayo, sisi wa-Tanzania tunapaswa kujifunza kutokana na makosa. Hii si mara ya kwanza watu wa nje kutangaza habari za nchi yetu kwa namna ambayo haitupendezi. Kwa mfano, tumelalamika kwa muda mrefu kuwa nchi jirani inatangaza kuwa Mlima Kilimanjaro uko kwao. Na sasa tunalalamikia hii taarifa ya Lonely Planet kuhusu Arusha. Je, tutalalamika mpaka lini? Je, tutaweza kushindana na hao wapinzani wetu kwa kulalamika tu?
Katika blogu zangu, na za wengine, na pia katika kitabu changu cha Changamoto, nimeandika tena na tena kuwa wa-Tanzania tuache uzembe. Tujibidishe katika elimu, ambayo ni pamoja na elimu ya lugha. Tuwe na uwezo wa kujieleza, kwa ufasaha na viwango vya juu kabisa, iwe ni kwa ki-Swahili au ki-Ingereza. Tuwe na tabia ya kununua na kusoma vitabu, kujiongezea maarifa na ujuzi, pamoja na ujuzi wa lugha.
Njia madhubuti ya kupambana na propaganda hizi tunazozilalamikia ni sisi wenyewe kuandika habari za nchi yetu na kuzisambaza duniani. Katika dunia ya leo, ya utandawazi na tekinolojia ya mawasiliano ya mtandaoni, uwanja uko wazi kwetu sote. Tutumie fursa hizi kama wanavyozitumia hao tunaowalalamikia.
Kama kweli tunaudhika na yale tunayofanyiwa, njia iliyopo ni hii ya kujibu mapigo. Binafsi, najitahidi kuandika habari zetu, kama njia moja ya kuipa dunia mtazamo wa m-Tanzania. Ninaandika kuhusu wa-Tanzania na wa-Afrika, kuhusu u-Tanzania na u-Afrika, ili kupambana na hao waliojivika kofia ya kuwa wasemaji wetu, wakati hatujawapa wadhifa huo.
Kampuni ya Lonely Planet ni kubwa sana duniani, ambayo vitabu vyake vinasomwa na watu zaidi ya 900,000. Mimi ni mtu moja tu, na sina mtandao na nguvu za kiuchumi namna hiyo. Lakini, hii sio sababu ya kukata tamaa. Cha msingi ni kujiamini. Wahenga walituachia busara katika methali zao. Walituambia, kwa mfano, kuwa mwanzo wa makubwa ni madogo na pia bandu bandu humaliza gogo.
Juzi tu kwenye blogu hii, bofya hapa, nilimnukuu msomaji wangu mmoja akisema kuwa kitabu cha Africans and Americans alikiona kuwa bora zaidi kuliko cha Lonely Planet. Pamoja na hali yangu ya chini sana nikifananisha na Lonely Planet, sina wasi wasi kuwa kadiri siku zinavyopita, nitalipunguza hili gogo liitwalo Lonely Planet.
Walichoandika Lonely Planet kuhusu Arusha kiwe ni changamoto kwetu wa-Tanzania, kwamba tusikae tunalalamika tu. Tupambane nao kwa vitendo.
Inaeleweka kwa nini wahusika wa mji wa Arusha na labda wa-Tanzania wengi wanaishutumu taarifa hii ya Lonely Planet. Mji wa Arusha unajulikana kwa utalii, na katika ushindani uliopo duniani, wahusika wote wanajitahidi kuwa na jina zuri, ili wafanikiwe kibiashara.
Pamoja na yote hayo, sisi wa-Tanzania tunapaswa kujifunza kutokana na makosa. Hii si mara ya kwanza watu wa nje kutangaza habari za nchi yetu kwa namna ambayo haitupendezi. Kwa mfano, tumelalamika kwa muda mrefu kuwa nchi jirani inatangaza kuwa Mlima Kilimanjaro uko kwao. Na sasa tunalalamikia hii taarifa ya Lonely Planet kuhusu Arusha. Je, tutalalamika mpaka lini? Je, tutaweza kushindana na hao wapinzani wetu kwa kulalamika tu?
Katika blogu zangu, na za wengine, na pia katika kitabu changu cha Changamoto, nimeandika tena na tena kuwa wa-Tanzania tuache uzembe. Tujibidishe katika elimu, ambayo ni pamoja na elimu ya lugha. Tuwe na uwezo wa kujieleza, kwa ufasaha na viwango vya juu kabisa, iwe ni kwa ki-Swahili au ki-Ingereza. Tuwe na tabia ya kununua na kusoma vitabu, kujiongezea maarifa na ujuzi, pamoja na ujuzi wa lugha.
Njia madhubuti ya kupambana na propaganda hizi tunazozilalamikia ni sisi wenyewe kuandika habari za nchi yetu na kuzisambaza duniani. Katika dunia ya leo, ya utandawazi na tekinolojia ya mawasiliano ya mtandaoni, uwanja uko wazi kwetu sote. Tutumie fursa hizi kama wanavyozitumia hao tunaowalalamikia.
Kama kweli tunaudhika na yale tunayofanyiwa, njia iliyopo ni hii ya kujibu mapigo. Binafsi, najitahidi kuandika habari zetu, kama njia moja ya kuipa dunia mtazamo wa m-Tanzania. Ninaandika kuhusu wa-Tanzania na wa-Afrika, kuhusu u-Tanzania na u-Afrika, ili kupambana na hao waliojivika kofia ya kuwa wasemaji wetu, wakati hatujawapa wadhifa huo.
Kampuni ya Lonely Planet ni kubwa sana duniani, ambayo vitabu vyake vinasomwa na watu zaidi ya 900,000. Mimi ni mtu moja tu, na sina mtandao na nguvu za kiuchumi namna hiyo. Lakini, hii sio sababu ya kukata tamaa. Cha msingi ni kujiamini. Wahenga walituachia busara katika methali zao. Walituambia, kwa mfano, kuwa mwanzo wa makubwa ni madogo na pia bandu bandu humaliza gogo.
Juzi tu kwenye blogu hii, bofya hapa, nilimnukuu msomaji wangu mmoja akisema kuwa kitabu cha Africans and Americans alikiona kuwa bora zaidi kuliko cha Lonely Planet. Pamoja na hali yangu ya chini sana nikifananisha na Lonely Planet, sina wasi wasi kuwa kadiri siku zinavyopita, nitalipunguza hili gogo liitwalo Lonely Planet.
Walichoandika Lonely Planet kuhusu Arusha kiwe ni changamoto kwetu wa-Tanzania, kwamba tusikae tunalalamika tu. Tupambane nao kwa vitendo.
Wednesday, March 10, 2010
Mteja Anapofurahi
Leo mama moja Mmarekani ameniandikia ujumbe kwenye ukurasa wangu wa Facebook. Anaelezea kuhusu kitabu changu cha Africans and Americans, na jinsi kilivyomsaidia alipokuwa Afrika Mashariki:
I remember being glad I had read it. Observations from someone who has lived in both Minnesota and East Africa, and a scholar no less, were a lot more insightful than my Lonely Planet.
Ni faraja kwangu kupata maoni ya wasomaji. Ni furaha kuwasikia kuwa wameridhika. Niliandika kitabu kwa sababu niliona kuna tatizo duniani lililohitaji ufumbuzi, tatizo la maelewano baina ya watu wa tamaduni mbali mbali. Lengo langu halikuwa kujipatia pesa. Hii Lonely Planet anayoitaja ni kampuni maarufu inayochapisha vitabu kwa ajili ya wasafiri. Vitabu hivi vinaelezea taarifa za nchi mbali mbali. Basi, nimetabasamu kusoma kauli ya huyu mama, kuwa kitabu changu ni tishio kwa Lonely Planet. Wakae chonjo.
Ni kweli kuwa watu wananunua kitabu hiki. Na mimi nazingatia hilo. Lakini jambo la msingi zaidi kwangu ni kuwa mteja aridhike. Asione kuwa alipoteza hela zake au kitu alichonunua hakikumridhisha. Mteja anapofurahi kama huyu wa leo, nami nafurahi.
Mara kwa mara, huwa naalikwa kwenda kutoa mihadhara kuhusiana na kitabu hiki au maandishi yangu mengine. Kama ilivyo kawaida hapa Marekani, wanaonialika wananiuliza gharama ya mihadhara yangu ni kiasi gani.
Ningekuwa mtu ninayeweka pesa mbele, ningesema hii ni fursa yangu ya kuwakomoa na kutajirika. Lakini mimi, pamoja na mahitaji mengi ya pesa ambayo sote tunayo, siwezi kufanya hivyo. Kwa nini nifanye jambo ambalo haliendani na dhamiri yangu? Sipendi makuu, na sikulelewa katika mkondo wa kujilimbikizia utajiri.
Ninaridhika na malipo ya wastani. Vile vile, hata kama taasisi au jumuia inayonialika haina pesa, mimi huwa naenda kuwapa mhadhara. Akili niliyo nayo nilipewa na Mungu, haikuwa haki yangu, wala siwezi kujivunia. Nina wajibu wa kuitumia kwa manufaa ya wanadamu, si kwa manufaa yangu binafsi. Ninaamini kuwa nikifanya ubinafsi, Mungu anaweza kuninyang'anya.
Furaha ya mteja ni malipo tosha kwa juhudi zangu, na ni njia ya kumtukuza Mungu aliyenipa uwezo.
I remember being glad I had read it. Observations from someone who has lived in both Minnesota and East Africa, and a scholar no less, were a lot more insightful than my Lonely Planet.
Ni faraja kwangu kupata maoni ya wasomaji. Ni furaha kuwasikia kuwa wameridhika. Niliandika kitabu kwa sababu niliona kuna tatizo duniani lililohitaji ufumbuzi, tatizo la maelewano baina ya watu wa tamaduni mbali mbali. Lengo langu halikuwa kujipatia pesa. Hii Lonely Planet anayoitaja ni kampuni maarufu inayochapisha vitabu kwa ajili ya wasafiri. Vitabu hivi vinaelezea taarifa za nchi mbali mbali. Basi, nimetabasamu kusoma kauli ya huyu mama, kuwa kitabu changu ni tishio kwa Lonely Planet. Wakae chonjo.
Ni kweli kuwa watu wananunua kitabu hiki. Na mimi nazingatia hilo. Lakini jambo la msingi zaidi kwangu ni kuwa mteja aridhike. Asione kuwa alipoteza hela zake au kitu alichonunua hakikumridhisha. Mteja anapofurahi kama huyu wa leo, nami nafurahi.
Mara kwa mara, huwa naalikwa kwenda kutoa mihadhara kuhusiana na kitabu hiki au maandishi yangu mengine. Kama ilivyo kawaida hapa Marekani, wanaonialika wananiuliza gharama ya mihadhara yangu ni kiasi gani.
Ningekuwa mtu ninayeweka pesa mbele, ningesema hii ni fursa yangu ya kuwakomoa na kutajirika. Lakini mimi, pamoja na mahitaji mengi ya pesa ambayo sote tunayo, siwezi kufanya hivyo. Kwa nini nifanye jambo ambalo haliendani na dhamiri yangu? Sipendi makuu, na sikulelewa katika mkondo wa kujilimbikizia utajiri.
Ninaridhika na malipo ya wastani. Vile vile, hata kama taasisi au jumuia inayonialika haina pesa, mimi huwa naenda kuwapa mhadhara. Akili niliyo nayo nilipewa na Mungu, haikuwa haki yangu, wala siwezi kujivunia. Nina wajibu wa kuitumia kwa manufaa ya wanadamu, si kwa manufaa yangu binafsi. Ninaamini kuwa nikifanya ubinafsi, Mungu anaweza kuninyang'anya.
Furaha ya mteja ni malipo tosha kwa juhudi zangu, na ni njia ya kumtukuza Mungu aliyenipa uwezo.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...
-
Ukizunguka mitaani Dar es Salaam, utakuta matangazo mengi ya waganga wa kienyeji. Waganga hao wanatoka sehemu mbali mbali, kama vile Sumbaw...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Jina la Shaaban Robert ni maarufu miongoni mwa wa-Tanzania na wengine wa nchi zingine wanaokijua ki-Swahili. Lakini, tujiulize ni wa-Tanza...