Saturday, April 10, 2010

Mpambano na Lonely Planet

Siku kadhaa zilizopita niliandika kuhusu msomaji wa kitabu changu cha Africans and Americans ambaye alisema kinafaa kuliko kile cha Lonely Planet. Bofya hapa. Nilitamka kiutani kuwa Lonely Planet wakae chonjo, maana wamepata mshindani.

Lakini baadaye, nililazimika kuandika tena kuhusu Lonely Planet, baada ya wao kuandika taarifa iliyoudhalilisha mji wetu wa Arusha. Bofya hapa. Hapo uzalendo ulinisukuma kusema kuwa hao sasa wanatuchokoza, na lazima tujizatiti kujibu mapigo.

Dada Subi, ambaye ni mfuatiliaji makini wa maandishi ya wanablogu wa Bongo na pia mshauri wetu tunayempenda na kumheshimu sana, kanibonyeza leo asubuhi kuwa kuna jambo limetokea Lonely Planet, yaani mteja anayepangia kwenda Tanzania anaulizia kitabu au vitabu vya kusoma, ambavyo si vya aina ya Lonely Planet.

Basi, hapo nimeona lazima niingie mzigoni na kuwachangamkia hao Lonely Planet. Sio kuwalazia damu; ni kuwavalia njuga tu. Nimefanya hivyo tayari, kwa kumpa yule mteja taarifa anazohitaji. Bofya hapa. Heshima na shukrani kwa Dada Subi, kama kawaida, na blogu yake maarufu hii hapa.

3 comments:

MARKUS MPANGALA said...

hii ni vita kali, ngoja tuone matokeo

Mbele said...

Mwaka huu hapatakalika. Kaa mkao wa kula :-)

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Kaazi kweli kweli!

hakuna kulala mpaka kieleweke!

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...