Thursday, April 1, 2010

Warsha Zangu Tanzania, 2010

Niko katika maandalizi ya kuendesha warsha Tanzania, kama nilivyofanya mwaka jana na mwaka juzi. Kwa taarifa fupi, bofya hapa na hapa. Maandalizi yanakwenda vizuri, na hadi leo, kwa kutumia mawasiliano ya barua pepe, nimeshapanga ratiba hii:

Juni 12, 2010, warsha kuhusu, "Culture and Globalization," Meeting Point Tanga.

Julai 3, 2010, warsha kuhusu, "Culture and Globalization," Arusha Community Church.

Julai 10, 2010, warsha kuhusu, "Cultural Tourism," Arusha Community Church.

Niko katika mawasiliano na wadau wa Zanzibar, ili kuandaa warsha Visiwani. Taarifa nitaleta baadaye. Nafanya mpango wa warsha Dar es Salaam pia.

Warsha hizi zitaendeshwa kwa ki=Ingereza, kama siku zilizopita, kwa sababu wahudhuriaji huwa wa mataifa mbali mbali. Yeyote anakaribishwa.

Nina mengi yanayonisukuma kuja kuendesha warsha hizi Tanzania. Kadiri ninavyotoa mihadhara huku ughaibuni, katika vyuo, taasisi, makampuni, na mashirika kuhusu athari za tofauti za tamaduni duniani, nazidi kutambua kuwa waTanzania tutapata shida katika dunia hii ya utandawazi kama hatufanyi juhudi ya kujielimisha na kujiandaa.

Haijalishi kama wewe ni mwanadiplomasia, mfanyabiashara, mwanafunzi, mmiliki wa shule, mfanya kazi katika kampuni, au mtafiti. Katika dunia ya leo, hatuwezi kukwepa kukumbana na watu wa tamaduni tofauti, na bila kuelewana, tutaishia katika migogoro na kuyumba au kuharibika kwa yale tunayotegemea kuyafanikisha. Mifano ni mingi duniani kote, na nchi mwetu pia.

Warsha hizi ni fursa si tu ya kunisikiliza mimi na kuniuliza masuali, bali pia fursa ya washiriki kufahamiana. Kwa hivi, nawahimiza wahudhuriaji kuja na taarifa za shughuli zao, iwe ni biashara, au shughuli nyingine yoyote. Ni njia nzuri ya kujitangaza na kujijengea mtandao. Nami nitaleta taarifa zangu, pamoja na vitabu vyangu.

Ninafanyia warsha hizi Tanzania, kama kianzio tu, lakini mkakati wangu ni kuzipeleka katika nchi zingine za jirani, nikianzia na Kenya. Hatimaye nataka kufanya warsha hizi katika nchi mbali mbali za Afrika na kwingineko, kwani elimu haijui mipaka ya nchi.

Kwa taarifa zaidi, na pia kujisajili kwa warsha, andika ujumbe: info@africonexion.com. Kama unataka kununua vitabu vyangu Tanzania, piga simu 0717 413 073 au 0754 888 647.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...