Showing posts with label Mbaraka Mwinshehe. Show all posts
Showing posts with label Mbaraka Mwinshehe. Show all posts

Sunday, August 9, 2015

Shaaban Robert na Mbaraka Mwinshehe Waliongelea Umuhimu wa Shule

Nikiachilia mbali jinsi wazazi wangu walivyohimiza elimu, nikiachilia mbali jinsi Mwalimu Nyerere alivyohimiza elimu, naukumbuka kwa namna ya pekee mchango wa mwandishi Shaaban Robert na mwanamuziki Mbaraka Mwinshehe katika kuhimiza elimu.

Ninakumbuka jinsi baba yangu, nilipokuwa shule ya msingi, alivyokuwa ananitia msukosuko iwapo nilishindwa kupata 100% katika zoezi lolote au mtihani wowote. Ninakumbuka pia jinsi Mwalimu Nyerere alivyokuwa anahimiza elimu, kwa watu wote, kuanzia watoto hadi wazee, kama nilivyowahi kuandika katika blogu hii.

Shaaban Robert ni mtu anayenifanya nimkumbuke baba yangu. Nilijionea hayo niliposoma kitabu kiitwacho Barua za Shaaban Robert, ambacho habari zake niliziandika katika blogu hii. Humo tunaona jinsi Shaaban Robert alivyokuwa anamhamasisha mdogo wake Yusuf Ulenge afanye bidii katika elimu, akimtimizia mahitaji yote ya shule. Kwa wazazi na walezi, Shaaban Robert ni mfano wa kuigwa.

Mbaraka Mwinshehe, mwanamuziki ambaye wakati wa ujana wangu alitingisha Afrika Mashariki, ya Kati, na Kusini kwa nyimbo na muziki wake, aliimba wimbo maarufu wa kuwaasa vijana wazingatie elimu. Wimbo huo, "Enyi Vijana Sikilizeni," unaweza kuusikiliza hapa:

https://archive.org/details/EnyiVijanaSikilizeni

Friday, August 13, 2010

Niko Morogoro: Mji Kasoro Bahari

Nimekuwa Morogoro tangu juzi, nikipunga upepo na kutembelea sehemu kadhaa.

Morogoro ni mji maarufu katika Tanzania. Uko katika njia kuu za usafiri baina ya Tanzania na nchi za Afrika ya kati na kusini.
Ni mji uliosifiwa sana na mwanamuziki maarufu Mbaraka Mwinshehe, kwa uzuri wake, na uzuri wa mandhari yake. Katika sifa hizi, aliongelea jinsi maji yanavyotiririka milimani Morogoro. Wenyeji wa hapo, wa-Luguru, ni maarufu miongoni mwa sisi watani zao, kwa jinsi nao wanavyojivunia huu mji, wanaouita Mji Kasoro Bahari.

Kila ninapopita Morogoro, nakumbuka umaarufu wake. Hapo kuna shule na vyuo maarufu tangu zamani, kama vile Kilakala, Kigurunyembe, Mzumbe, na Sokoine. Miaka ya karibuni kimeanzishwa pia chuo kikuu cha Ki-Islam. Ni mji muhimu kwa upande huu, wa elimu.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...