Showing posts with label uchambuzi. Show all posts
Showing posts with label uchambuzi. Show all posts

Thursday, October 19, 2017

"Men Made Out of Words" ( Wallace Stevens)

Wallace Stevens ni mmoja wa washairi maarufu wa Marekani. Mara ya kwanza kupata fursa ya kuyasoma mashairi yake ni nilipokuwa ninasomea shahada ya uzamifu katika huo kikuu cha Wisconsin-Madison,1980-86. Nilichukua kozi kadhaa katika idara ya ki-Ingereza, mojawapo ikiwa "Poetry." Alitufundisha profesa John Brenkman.

Profesa Brenkman alikuwa na mtindo wa kufundisha ambao ulilifanya somo la "Poetry" livutie. Kwa uzoefu wangu wa kabla ya hapo, katika kusoma Tanzania, ushairi wa ki-Ingereza ndilo lilikuwa somo gumu kuliko mengine. Nilidokeza jambo hilo katika kijitabu changu cha Notes on Okot p Bitek's Song of Lawino.

Tangu nilipofundishwa na Profesa Brenkman, jina la Wallace Stevens limekuwa linanivutia, na daima niko tayari kusoma mashairi yake. Huu ni ushahidi wa jambo ambalo linafahamika vizuri, yaani namna mwalimu bora anavyoweza kumwathiri mwanafunzi. Jana nimeangalia kitabu changu cha mashairi, The Voice That is Great Within Us, na shairi moja lililonivutia ni "Men Made Out of Words," la Wallace Stevens. Ni shairi ambalo limeandikwa kwa uchache wa maneno na tamathali za usemi, na falsafa yake inachangamsha bongo.

MEN MADE OUT OF WORDS (Wallace Stevens)

What should we be without the sexual myth,
The human revery or poem of death?

Castratos of moon-mash--Life consists
Of propositions about life. The human

Revery is a solitude in which
We compose these propositions, torn by dreams,

By the terrible incantations of defeats
And by the fear that defeats and dreams are one.

The whole race is a poet that writes down
The eccentric propositions of its fate.


Thursday, August 26, 2010

Ujumbe wa Msomaji wa Kitabu

Naichukulia blogu hii kama mahali ambapo naweka mambo yangu binafsi: kumbukumbu, fikra, dukuduku, hisia na kadhalika. Ingawa najua watu wanasoma ninayoandika, siwezi kusema kuwa wao ndio walengwa. Ninajiandikia mwenyewe, kwa uhuru na namna ninayotaka, mambo yangu binafsi.

Leo nimepata ujumbe kutoka kwa mshiriki mmojawapo wa warsha niliyoendesha Dar es Salaam mwaka jana. Bofya hapa. Ameniulizia naenda lini kutoa warsha zingine akahudhurie.

Pia amesema kuwa kitabu cha Africans and Americans ambacho alikinunua wakati wa warsha kinamsaidia katika kutoa mihadhara na kushughulikia masuala mengine ya mahusiano sehemu za kazi.

Ni wazi nimefurahi kusikia hayo. Nani asingefurahi? Nimemwambia nafarijika kuwa kitabu kimezaa matunda mema kwake, hasa nikikumbuka gharama ya warsha na kitabu. Lengo moja la kuandika kitabu hiki lilikuwa kuwasaidia wanaohitajika kutoa mihadhara kuhusu tofauti za tamaduni na matatizo na changamoto zitokanazo na tofauti hizi. Wengine wanakuwa na majukumu ya kusuluhisha migogoro. Mimi mwenyewe nakitumia kitabu hiki, mahali pa kuanzia.

Maoni ya wasomaji ni msaada mkubwa kwa mwandishi. Nami nina bahati ya kuyapata mara kwa mara. Wengine, kama ilivyo katika ulimwengu wa vitabu, wanayaweka maoni yao hadharani, kama haya hapa. Nawajibika kutoa shukrani.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...