Saturday, February 12, 2022

MTanzania Ughaibuni Aongelea Kitabu cha "Matengo Folktales"

 

Wiki za hivi karibuni nimepata kufahamiana na dada Corona Cormak, mTanzania aishiye Jamhuri ya Czech. Ni mwandishi mahiri wa vitabu vya watoto, ambavyo nimesoma nikavifurahia. Pia ni msimuliaji hodari wa hadithi.

Wiki hii, katika ukurasa wake wa Instagram, Coriona ameandika uchambuzi wake wa kitabu changu Matengo Folktales. Ameandika hivi:

I will start with a big smile. This book Matengo Folktales by John Mbele @africonexion. Took me way back into those days of story telling. Three stories in this book were so vividly. The Monster in the Rice, The Tale of two women and the Tale of Katigija. The sound of the songs in these stories is what I am still trying to remember. These songs were always sang with everyone when the stories were narrated. This is what is missing in story telling these days. We let our children just listen to the story without them taking part.

However, I am quite shocked with the amount of killing in every story. At least I don't remember the killing part. For example the Tale of two women, I remember this part when the woman was told to lick the wounds. And in Katigija Tale I remember the grandma singing when she brought the food to the child and the Monster in the Rice field, I remember how the children kept on disappearing.

My son was shocked when I told him The tale of Monster in the Rice. He was like, what a story, what a family 🙈🤣
Beautiful written and I like the comment section. This helps one to understand why these stories were what they were.
Now I need someone to sing those songs for me 🥳🤗
 
Tafsiri ya juu juu ya kiSwahili ni hivi:

Nitaanza na tabasamu kubwa. Kitabu ni "Matengo Folktales" cha [Joseph] Mbele. Kilinirudisha kwenye siku zile za usimuliaji hadithi. Hadithi tatu katika kitabu hiki zilisisimua: “Jitu Katika Shamba la Mpunga,” “Kisa cha Wanawake Wawili” na "Hadithi ya Katigija.” Najaribu kukumbuka sauti za nyimbo katika hadithi zile. Nyimbo hizi daima ziliimbwa na wote wakati hadithi zinasimuliwa. Hicho ndicho kinachokosekana katika usimulizi wa hadithi leo. Tunawafanya watoto wetu wasikilize tu bila wao kushiriki.

Lakini, nimeshtushwa na idadi ya mauaji katika kila hadithi. Sikumbuki sawasawa sehemu ambapo mauaji yenyewe yanatokea. Kwa mfano, "Kisa cha Wanawake Wawili," nakumbuka pale mwanamke anapoambiwa kulamba vidonds. Na katika “Hadithi ya Katigija” nakumbuka bibi anavyoimba wakati anamletea mtoto Katigija chakula, na katika “Jitu Katika Shamba la Mpunga” nakumbuka jinsi watoto walivyokuwa wanapotea. Mtoto wangu alishtuka nilipomsimulia “Kisa cha Jitu Katika Shamba la Mpunga.” Alishangaa ni hadithi gani hiyo, na ni familia gani hiyo.
 
Kitabu kimeandikwa vizuri na nilipendezwa na maelezo kuhusu hadithi. Yanasaidia kuelewa kwa nini hadithi ziko zilivyo. Sasa nahitaji mtu wa kuniimbia nyimbo zilozomo.

 

 

Wednesday, February 9, 2022

Vitabu Viko Chuoni Mbeya

 

Tarehe 27 hadi 29 Januari, 2022, nilikuwa mgeni wa Catholic University College of Mbeya. Nilikuwa nimealikwa kutoa mhadhara juu ya “Africans and Americans: Embracing Cultural Differences.” Lakini nilijikuta katika shughuli zingine pia, ikiwemo mazungumzo na waalimu na pia mkuu wa chu

 

Katika mhadhara wangu, niliibua masuala ambayo nimeyaongelea katika vitabu vyangu Africans and Americans: Embracing Cultural Differences na Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Lengo langu kuu lilikuwa kuanzisha jadi ya kutafakari changamoto za tofauti za tamaduni katika ulimwengu wa utandawazi wa leo.

Tafakari hii inapaswa iwe endelevu. Kuchangia hilo, nilikabidhi nakala za hivi vitabu vyangu viwili kwa ajili ya maktaba ya chuo. Baadaye mkurugenzi  wa maktaba ameniandikia ujumbe wa shukrani kwa kupewa vitabu hivyo. 

Saturday, December 25, 2021

Krismasi Katika Fasihi

Pamoja na mambo mengine, fasihi inaweza kubeba tafakari au taswira ya yale tunayokutana nayo maishani.Leo, siku ya Krismasi, napenda kuanzisha tafakari juu ya fasihi na Krismasi. Kwa upande wangu, kazi za fasihi ninazozikumbuka wakati huu wa Krismasi ni hizi:

1) "A Christmas Carol" (hadithi ya Charles Dickens)
2) "Journey of the Magi" (shairi la T.S. Eliot)
3) "Christ Climbed Down" (shairi la Lawrence Ferlinghetti)

Kazi hizi zote zina mambo mengi yanayohusu Krismasi na pia yanayogusa hisia kwa umahiri wa sanaa. KiIngereza kilivyotumika katika "Journey of the Magi," kwa mfano, kinagusa sana, na ubunifu wa simulizi yake ni wa kusisimua. Ninajiona mwenye bahati kuifahamu lugha hiyo vizuri sana, kwa undani kabisa, na ninafaidi uhondo.

Kwa upande mwingine, shairi la Ferlinghetti linasisimua kwa jinsi linavyokejeli kugeuzwa kwa Krismas kuwa si tukio la kidini bali la kibiashara. Kwa maana hiyo, Ferlinghetti anatukumbusha yale waliyoandika akina Marx na Engels katika "Communist Manifesto" kuhusu namna ubepari unavyohujumu na kunajisi mambo mbali mbali.

Huu ni wakati wa muafaka kwa wapenzi wa fasihi kutafuta tungo hizi, na zingine, kuzisoma au kurudia kuzisoma, na kuzitafakari.

Thursday, November 11, 2021

Msomaji na Mpiga Debe Wangu Aikwaa Tuzo

Jana niliandika taarifa za msomaji na mpiga debe wangu Joy Zenz, mKenya aishiye uJerumani.

Napenda niseme kuwa juhudi zake za kuwaunganisha akina mama waAfrika waliko Ulaya na kwingineko na kuwahamasisha katika masuala ya maendeleo kwao na kwa bara la Afrika yamemfanya atambuliwe na kutuzwa kwa namna mbali mbali.

Leo nimeona taarifa kuwa ameikwaa tuzo muhimu ya Global Africa Awards. Nimefurahi na ninampongeza kwa dhati msomaji wangu huyu na mpiga debe.

Tuesday, November 9, 2021

WaKenya Wazidi Kukinadi Kitabu


Nimewahi kuandika mtandaoni tena na tena nikiwasifu na kuwashukuru waKenya kwa jinsi walivyokuwa bega kwa bega nami katika utafiti na uandishi wangu.

Huku Marekani, waKenya wamekuwa wasomaji na wapiga debe wangu wakuu kama nilivyotamka, kwa mfano, hapa na hapa.

Sasa amejitokeza mKenya mwingine, Joy Awe, aishiye uJerumani. Yeye ni mwanzilishi na mratibu wa jumuia iitwayo African Women in Europe.

Ameweka picha zake mtandani akiwa na kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, pamoja na ujumbe huu:

Highly recommended book to read especially diaspora or anyone wanting to do business in Africa. Available on Amazon.

Naendelea kuwashukuru waKenya kwa mshikamano nami.

Sunday, November 7, 2021

Simulizi za Wanawake waAfrika Waishio Ulaya


Ninaandika ujumbe huu nikiwa ninavisubiri vitabu viwili vya wanawake waAfrika waishio Ulaya. Napenda nielezee jinsi nilivyopata taarifa za vitabu hivi.

Tarehe 31 Mei hadi 4 Juni mwaka huu nilishiriki mkutano mkubwa mtandaoni, "Trade With Africa Business Summit." Mwandaaji, Toyin Umesiri, alikuwa ameniomba nikazungumzie kitebu changu kiitwacho Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Nilifanya hivyo, nikijikita katika kuongelea vipengele vya tamaduni vinavyohitaji kuzingatiwa katika biashara baina ya waAfrika na waMarekani.


Kwenye mkutano ule, nilipata kufahamiana na mtoa mada Joy Wanjiru Zenz, mama mKenya aishiye uJerumani na ni mwanzilishi na mwendeshaji wa jumuia ya wanawake waAfrika waishio Ulaya. Alishuhudia jinsi kitabu changu kilivyokuwa kinatajwa na baadhi ya washiriki wa mkutano.

Siku kadhaa baada ya mkutano, Joy nami tuliwasiliana,  akanieleza kuwa wanajumuia wake wamechapisha vitabu kuhusu maisha yao Ulaya. Nilivutiwa na taarifa hii. Ninayafahamu maisha ya waAfrika Marekani, lakini si Ulaya. Ilibidi nimwambie Joy kuwa ninahitaji vitabu hivi. Ninavisubiri kwa hamu.

Saturday, November 6, 2021

Msomaji Wangu Mpya, mTanzania wa Czech

Wiki hii ya kwanza ya Novemba, 2021, nimemmpata msomaji mpya, Corona Cermak, mTanzania aishiye Jamhuri ya Czech. Nilisikia jina lake kwa mara ya kwanza kutoka kwa dada Joy Wanjiru Zenz, mKenya aishiye uJerumani, ambaye aliniambia kuwa kuna huyu mTanzania mwandishi aishiye Czech.

Katika kufuatilia Facebook, YouTube, na Instagram, nimeona shughuli za Corona, za ufundishaji wa kiSwahili na uandishi wa vitabu vya watoto. Vitabu alivyochapisha ni The Rooster's VoiceSauti ya Jogoo, na Grandma Pipi and the Roses.

Juzi nilimwandikia kuwa nimeagiza vitabu vyake Amazon, naye hima akaniletea picha akiwa ameshika kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. alichoagiza hivi karibuni mtandaoni.

Mara tu baada ya kukipata kitabu changu, amekisoma na kukiongelea mitandaoni Instagram na Facebook akiwahimiza watu waendao Marekani, Ulaya, na Tanzania wakisome. Amesema pia kuwa ameagiza kitabu changu cha Matengo Folktales. Ni bahati njema kufahamiana na mwalimu na mwandishi mwenzangu, mTanzania aishiye ughaibuni. Tunategemea kubadilishana mawazo na uzoefu.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...