 Tarehe 29 September hadi 1 Oktoba, palifanyika mkutano wa Africa Network, hapa chuoni St. Olaf. ambapo ninafundisha. Africa Network ni jumuia ya vyuo vyenye kujihusisha na uendelezaji wa masomo kuhusu Afrika, katika taaluma mbali mbali. Jumuia hiyo ilianzishwa mwaka 2004 na watu wachache  kutoka vyuo mbali mbali, na mwaka hadi mwaka imekuwa ikivutia watu kutoka vyuo vingine.
Tarehe 29 September hadi 1 Oktoba, palifanyika mkutano wa Africa Network, hapa chuoni St. Olaf. ambapo ninafundisha. Africa Network ni jumuia ya vyuo vyenye kujihusisha na uendelezaji wa masomo kuhusu Afrika, katika taaluma mbali mbali. Jumuia hiyo ilianzishwa mwaka 2004 na watu wachache  kutoka vyuo mbali mbali, na mwaka hadi mwaka imekuwa ikivutia watu kutoka vyuo vingine.Katika mkutano wetu wa mwaka 2015, nilipendekeza kuwa mkutano wa mwaka huu ufanyike hapa chuoni St. Olaf. Kwa hivyo, nilibeba jukumu la kufuatilia kwa karibu kila kipengele cha maandalizi hayo, na hatimaye tumefanya mkutano kwa mafanikio makubwa.
Baadhi ya wahudhuriaji ni wa tangu zamani, lakini wengi walikuwa wapya. Tumefanikiwa kuwavuta watu kutoka vyuo vya mbali, hadi Afrika Kusini, ambao wako Marekani kwa wakati huu. Tumejifunza na tumefundishana mengi, na pia tumejengea mahusiano mapya yatakayotupeleka mbele katika shughuli zetu.
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment