Wednesday, May 29, 2019

Nimekutana na Mdau wa Kitabu Changu

Tarehe 19 Mei nilikwenda kukutana na mama Luanne Kallungi Skrenes katika mahafali ya 150 ya Luther Seminary. Mama huyu tumefahamiana kwa miaka kadhaa katika mtandao wa Facebook. Yeye ni mratibu wa programu ya kanisa la kiLuteri eneo la Michigan inayoendeleza mahusiano baina ya waLuteri wa Marekani na wenzao wa Tanzania.

Ni mpenzi wa kitabu changu, Africans and Americans:Embracing Cultural Differences, ambacho anakipendekeza kwa waMarekani wanaoenda Tanzania katika programu hiyo. . Yeye ni mratibu wa programu ya kupeleka waLuteri ya kupeleks watu Tanzania. Hata mwaka huu nilipoandaa warsha kuhusu "Culture and Globalization," aliwaandikia waTanzania anaofahamiana nao kuwahimiza wahudhurie. Kwa hayo yote, mama huyu amekuwa otu muhimu kwangu.

Tulifurahi kuonana. Nilifurahi kumwona mume wake, Askofu Thomas a Skrenes. Wote ni waongeaji wachangamfu. Niliwaambia kuwa ninaandika kitabu cha mwendelezo wa hicho cha kwanza, yaani "sequel," kwa kiIngereza. Mama aliniuliza kitaitwaje, nami nikamjibu "Chickens in the Bus." Tulicheka. Lakini hili ndilo jina la kitabu ninachoandaa.

Kati ya mambo ninayoyafurahia sana kama mwandishi ni kukutana na wasomaji na kusikia maoni yao kuhusu vitabu vyangu. Ni baraka kubwa kuwa na watu wenye moyo huu wa kunipa mrejesho, na ninawashukuru daima.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...