Friday, January 29, 2021

Africonexion Yashiriki KAN Festival

Kuanzia tarehe 28 hadi 30 Januari hii, kwenye kituo cha MS TCDC, Arusha, kunafanyika tamasha liitwalo KAN Festival. Kwa kuwa sikuweza kwenda kuhudhuria, niliwasiliana na ndugu Thomas Ratsim wa Arusha akaniwakilishe. Mwaka jana aliniwakilisha pia, na ninatumia jina la Africonexion: Cultural Consultants, ambayo ni kampuni ndogo niliyosajili mwaka 2002 hapa katika jimbo la Minnesota, Marekani. 

Shughuli za Africonexion: Cultural Consultants ni kutafiti, kuandika, na kuelimisha kuhusu za tofauti za tamaduni katika dunia ya utandawazi wa leo. Wateja ni wa aina nyingi, kama vile waMarekani wanaokwenda Afrika na waAfrika wanaofika Marekani, taasisi, makampuni, jumuia na vyuo. Lengo ni kuwawezesha watu kuelewa changamoto za tofauti za tamaduni ili kuboresha mahusiano na ufanisi katika shughuli.

Matamasha ni fursa ya kutangaza shughuli za Africonexion: Cultural Consultants, ikiwemo kwa njia ya vitabu na maongezi na watu wanaokuja kwenye meza yetu, na pia ni fursa za kujifunza kutoka kwa watu wanaohudhuria matamasha. Ni fursa za kubadilishana mawazo na uzoefu.
 

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...