Wednesday, January 27, 2021

Kitabu Kimefika Somalia

 Juzi tarehe 25, mama mmoja mSomali aishiye mjini Faribault hapa katika jimbo la Minnesota alinipigia simu. Nilikutana naye mara ya kwanza mwaka jana tamasha la kimataifa Faribault, nikampa nakala ya kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences.

Alivyonipigia jana alisema kuwa alikuwa amerejea kutoka safarini Somalia. Baada ya maongezi na fupi ya simu, aliniandikia ujumbe huu: Joseph, I forgot to tell you that I took your book to Somalia. The people loved reading your book. Yaani, Joseph, nilisahau kukuambia kuwa nilienda na kitabu chako Somalia. Watu walifurahia kusoma kitabu chako.

Nafurahi kuona jinsi kitabu hiki kinavyokubalika na waAfrika wa kila taifa, jinsia, dini, na kadhalika. Kuna vipengele fulani katika kitabu hiki ambavyo ninaposoma, ninapata wasi wasi kuwa huenda niliandika bila kuwaza kuwa kuna waIslamu Afrika. Ajabu ni kuwa waIslamu wenyewe hawajawahi kukwazika. Mmoja kati ya wasomaji wa kitabu hiki wa mwanzo kabisa alikuwa mama muIslamu msomi kutoka Ivory Coast. Alikipenda sana kitabu hiki. WaIslamu wengi wa Afrika, wakiwemo maprofesa wamevutiwa na kitabu hiki. Siku chache zilizopita, nilileta taarifa ya mSomali mwingine. Namshukuru Mungu kwa yote.



No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...