Sunday, September 19, 2021

Msomaji Amejipatia "Chickens in the Bus"

 

Jana, tarehe 18 Septemba, nilimpelekea msomaji anayeonekana nami pichani nakala ya kitabu changu kipya, Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Huyu mama, kutoka Togo, amekuwa msomaji wangu wa tangu zamani. Anavyo vitabu vyangu vya awali: Matengo Folktales na Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Mara aliposikia nimechapisha kitabu kingine, aliagiza nakala. 

Nina bahati ya kuwa na wasomaji makini namna hii. Huyu mama ni msomi na mzoefu katika idara ya ustawi wa jamii. Ninategemea kupata mrejesho adimu kutoka kwake atakapomaliza kusoma kitabu hiki.  

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...